KWA mara ya kwanza tangu aingie madarakani, Rais Jakaya Kikwete, anatarajiwa kushiriki katika mkutano wa nne wa Baraza la Biashara la Taifa (TNBC) utakaofanyika Desemba 11.
RIPOTI ya uchunguzi wa kifo cha raia, Bernad Mapunda, kilichotokana na kipigo cha polisi kwa tuhuma za wizi wa makasha 27 ya marumaru katika nyumba ya Kamanda wa Polisi wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Alfred Tibaigana, imetoka na hatua za kisheria zimekwishachukuliwa kwa askari aliyetoa kipigo hicho.
MAMLAKA ya Bandari Tanzania (TPA), imejivua lawama kwa kutoa ufafanuzi kwamba, udhaifu wa pampu za meli za mafuta ndiyo chanzo cha kudorora kwa kasi ya upakuaji mafuta kwenye mita maalum za mamlaka hiyo Kurasini (KOJ).
NAIBU Waziri wa Miundombinu, Dk Maua Daftari jana alifanya ziara ya ghafla katika Bandari ya Dar es Salaam na kubaini kwamba kuna meli mbili za mafuta zilizoingia nchini zikiwa hazina nyaraka za maelezo wala kuagizwa na wakala yeyote.