Wakati wa udogo safu hii ilizoea kuwasikia wazazi wakiongelea habari za TANU. Walikumbushana ahadi za mwana-TANU na miiko ya uongozi uzalendo na maendeleo ya jamii. Waliongelea ufugaji bora huku wakirejea na magazeti maarufu kama ukulima na ufagaji wa kisasa.
Hakuna ubishi kuwa nchi yetu imo matatani. Wala hakuna ubishi kuwa ufisadi upo tena kwa kiwango kikubwa. Ushahidi upo hata kama kuna watu wanaupuuzia. Nani haoni wanasiasa wanavyotajirika ghafla bila hata maelezo wala stahiki? Huyu ni kipofu hata kama ana macho.
Neno familia linaweza kutafsirika kutokana na mahali alipo mtu. Ukiongelea wazungu ni baba mama na mtoto au watoto. Ukiongelea waafrika ni zaidi ya hapo. Hata ukoo unaweza kuwa familia kama unaishi pamoja kwa misingi sawa kama ilivyo kwenye darasa la leo.
Rais mstaafu Benjamin Mkapa amekuwa bubu ghafla baada ya kuondoka madarakani! Hakuna aliyetegemea kuwa Mkapa bingwa wa kuandika hotuba ndefu na kuzodoa wapinzani wake angefikia hatua hii! Hakuna aliyetegemea Mkapa bingwa wa kujua kila jambo angedondoka chali hivi!
Wakati wa kudai uhuru, nchi yetu ilipata taabu sana kutokana na mfumo uliokuwa umewekwa na wakoloni. Wakoloni walipoivamia na kuikalia Afrika, walitumia mbinu nyingi chafu kuhakikisha wanaendelea kuinyonya.