JUMLA ya watu milioni nne wanatarajiwa kupimwa ukimwi hadi kufikia mwishoni mwa mwaka huu kupitia kampeni kubwa ya kitaifa inayozinduliwa leo na Rais Jakaya Kikwete.
“TUPO makini, tupo ndani ya wakati na tunaweza kutekeleza tuliyokusudia. tumesikia mengi yakichangiwa katika mjadala wa ofisi yangu, lakini ninachoweza kuwaeleza Watanzania ni kwamba maisha bora kwa kila Mtanzania yanawezekana.”
NCHINI Kenya, mwaka jana Gavana wa Benki Kuu ya nchi hiyo (KCB), Andrew Mullei, alishutumiwa kumtumia mtoto wake, Silla Mullei, kufanya kazi ndogo ya kitaalamu ya Benki Kuu.