WAZIRI wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, John Magufuli, amezijia juu halmashauri nchini na kuzitaka kuacha mara moja kuvunja nyumba za wananchi zilizojengwa katika maeneo ya makazi ambayo hayajapimwa.
LEO Wailamu kote nchini wameungana na wenzao duniani kusherehekea Sikukuu ya Idd el Hajj, mbayo husherehekewa baada ya mahujaji kukamilisha ibada ya hijja, kwenye miji mitakatifu ya Makka na Madina
KIWANGO cha kufaulu kwa wanafunzi wa darasa la saba kimeshuka kwa asilimia 16.3 mwaka huu ukilinganisha na mwaka jana, ambapo waliofaulu walikuwa asilimia 70.48 ya wanafunzi wote waliofanya mitihani.
UBALOZI wa Marekani nchini, umetaka Chama Cha Mapinduzi (CCM) na Chama cha Wananchi (CUF) kuhitimisha haraka na kwa haki mazungumzo ya kutafuta suluhu ya kudumu ya mpasuko wa kisiasa Zanzibar.
JUHUDI za serikali kuwasafirisha mahujaji waliokwama kwenda kuhiji Makka, zimeshindwa kuzaa matunda kwa wakati muafaka, baada ya ndege iliyokodiwa kutoka Kampuni ya AL-Wassam kushindwa kuhimili safari za kuwasafirisha mahujaji hao baada ya kuharibika.