MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana ilimfutia dhamana aliyekuwa Mkurugenzi wa Utumishi na Utawala wa Benki Kuu (BoT), Amatus Liyumba, ambaye ni mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya matumizi mabaya ya ofisi za umma na kusababisha hasara ya sh bilioni 221, baada ya kubaini kuwa aliidanganya mahakama.