MAKUNDI ya haki za binadamu nchini Israel, yamelishitumu jeshi la Israel kwa kuwatumia watoto wadogo wawili wa Kipalestina kama ngao ili kujizuia na mashambulizi yalitokea katika eneo la Ukingo wa Magharibi.
RAIS wa Marekani George W. Bush amepokelewa kwa maandamano yalioambatana na vurugu nchini Brazil kutokana na Marekani kuivamia Iraq na kusababisha vita nchini humo.
WAZIRI MKUU wa Iraq, Nouri al-Maliki amesema wiki mbili zijazo atafanya mabadiliko ya baraza lake la mawaziri ili kumaliza mgawanyiko wa makundi ya kikabila katika Serikali yake na kuleta umoja wa kitaifa.
LEO wananchi wa Ghana duniani kote pamoja na wapenda amani duniani wanasherehekea miaka 50 ya uhuru wa taifa hilo na kuweka rekodi ya kuwa taifa la kwanza la weusi barani Afrika kujipatia uhuru kutoka kwa dola ya Kiingereza, iliyokuwa inaporomoka baada ya kuwa kinara wa dunia kabla ya kuibuka kwa Marekani na Urusi.
POLISI nchini India imesema inawashikilia watu watatu wanaodaiwa kuhusika na ulipuaji wa treni ya abiria ya Samjhauta (Friendship) Express) iliyokuwa ikitokea India kuelekea Pakistan.