Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

 »  Home  »  Blogs  »  Serikali yawapiga tafu vijana wa Mafia
Marshy Abdu
Insured by Mafia Islanders You hit me!! We hit you!!! 

View all blogs by Marshy Abdu...
Serikali yawapiga tafu vijana wa Mafia
By Marshy Abdu | Published  07/24/2007
Wizara ya Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana imewadhamini vijana 15 wanaotoka wilaya ya Mafia mkoani Pwani na kupata mafunzo mafupi ya fani mbalimbali za ufundi.

Mafunzo hayo ya fani ya umeme, useremala, uashi, upishi, ushonaji na kilimo yamefanyika kwenye chuo cha maendeleo ya wananchi (FDC) wilayani Kisarawe, yamewajumuisha vijana hao wa mtaani.

Kwa mujibu wa Mkuu wa chuo hicho, Bw, Stephen Msanya, amesema lengo la kutoa mafunzo hayo yatawawezesha kuajiri wenyewe na kujiongezea kipato badala ya kukaa mtaani bila ya kuwa shughuli maalum na kuwa kishawishi cha kutenda maovu.

Amesema chuo hicho kimekuwa kikipokea wanafunzi wa aina mbalimbali ambao wamekuwa wakifundishwa kozi fupi kuanzia wiki mbili kama waliyopata wanafunzi hao na kuendelea hadi miaka miwili ili kuwaezesha kuwapa mwanzo wa kupata uelewa.

Bw, Msanya ameongeza pamoja na mafunzo hayo kuwa mafupi lakini yanaanza kuwapa mwanga wanafunzi hao na hata kuanza shughuli hizo japo si kwa kiwango kikubwa ambapo nyakati nyingine shughuli wazifanyazo huwapa kipato na kuja kujiunga tena na chuo hicho.

Kwa sasa chuo hicho kimekuwa kikitoza gharama ya sh 90,000 kwa mwaka kwa wanafunzi wa bweni kiwango ambacho kipo chini ili kusaidia wazazi wenye kipato kidogo kudunduliza fedha na kuwaleta vijana wao kujiunga.
Post a comment about this blog
Add comment
Comments


Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Nthelezi Nesaa
  4. Linda Garner
  5. Marshy Abdu
No popular authors found.