|
SERIKALI, kupitia Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, imetangaza vivutio vingi kwa vijana watakaojitokeza kujaza nafasi 3,500 za ualimu. Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Margaret Sitta, amesema hii ni nafasi pekee kwa vijana wenye sifa, kujitokeza kwa wingi kufaidika na fursa hiyo.
|