Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Waziri adai mbunge kikwazo cha maendeleo
Waziri adai mbunge kikwazo cha maendeleo
By Habari Tanzania | Published  09/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni na Michezo, Bw Mahmoud Thabit Kombo, amemtuhumu mbunge wa Jimbo la Mpendae kuwa ni kikwazo cha maendeleo kwenye Jimbo hilo.

Akizungumza na Nipashe jana, Waziri Kombo alimtaja mbunge huyo kuwa ni Bw. Issa Kassim Issa (CCM), na kwamba kila mara amekuwa kikwazo cha maendeleo jimboni hapo kwa kutoshirikiana na wananchi wake.

’’Huyu mbunge hana ushirikiano na wananchi wa jimbo lake? Amekuwa kikwazo cha maendeleo kwa kutoa ahadi hewa zisizotekelezeka,’’ alisema Waziri Kombo.

Kauli ya Naibu Waziri Kombo kumlaumu mbunge huyo, imekuja kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wanachama wa Ushirika wa Maendeleo ya Kinamama katika Jimbo hilo.

Wanawake hao walimlalamikia Mbunge Issa kwa kushindwa kuwapa Sh. 250,000 alizowaahidi katika kipindi cha kampeni za Uchaguzi Mkuu uliopita.

Alisema japokuwa yeye si mwanachama wa kikundi cha wanawake hao, anaona uchungu jinsi mbunge Issa anavyowazungusha kwa kutotimiza ahadi aliyowapa.

’’Kweli mbunge huyo anazorotesha maendeleo katika jimbo letu,’’ alisema Waziri Kombo.

Alipoulizwa juu ya shutuma hizo, Bw. Issa alisema nia yake ya kuwasaidia wananchi bado ipo pale pale, kinyume na madai ya baadhi ya wakazi wa jimbo hilo.

’’Ahadi yangu bado ipo pale pale na sababu ya kutotimiza ahadi niliyoahidi ni siri yangu binafsi, wala haina haja ya kutangazwa katika vyombo vya habari,’’ alisema mbunge Issa.

Aidha alisema Ushirika wa wanawake unatumiwa vibaya na baadhi ya wanasiasa wasiomtakia heri ndiyo maana wanaongea mambo wasiyoyajua.

Ushirika huo, unashughulika na kilimo cha umwagiliaji, biashara ndogo ndogo na ukodishaji wa vifaa katika shughuli mbali mbali za utamaduni na jamii.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.