Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kimataifa  »  Mambo yazidi kuwa magumu kwa Bush.
 »  Home  »  Nthelezi Nesaa  »  Mambo yazidi kuwa magumu kwa Bush.
Mambo yazidi kuwa magumu kwa Bush.
By Nthelezi Nesaa | Published  09/15/2006 | Habari za Kimataifa , Nthelezi Nesaa | Unrated
Na Mwanahabari wa HabariTanzania.com, Canada

Rais wa Marekani bwana George W. Bush anakabiliwa na mtihani mgumu baada ya chama chake cha Republican kuanza kumgeuka na kumpinga wazi wazi.

Hii imetokea wiki hii ambapo waziri wa zamani wa mambo ya nchi za nje chini ya utawala wa Bush,Generali mwenye nyota nne, Collins Powell kumtandika barua Rais Bush akipinga sera nzima ya ukamataji na kuhoji watuhumiwa wa ugaidi.

Collins amerejea tena kuhimiza kupinga kwake zoezi zima la kuzuilia watuhumiwa wa ugaidi kwenye kambi ya Guantanamo. Hii ni kutokana na kufanya hivyo kuvunja ibara ya tatu ya Mkataba wa Geneva (Geneva convention) ambao unasema kuwa wahalifu au watuhumiwa watendewe kibinadamu.

Wakati barua hiyo ya Powell vumbi lake halijatua,Bush alipata pigo jingine baada ya wabunge vikaka wa chama chake kumpinga wazi wazi wakiongozwa na Senata John McCain ambaye ni shujaa wa zamani wa vita.

Pamoja na mtoto wa nyumbani kama wanavyomuita waziri wa sasa wa mambo ya kigeni, Dr. Condolezza Rice, kuja na barua ya kujibu barua ya Powell, Bush alibaki hana la kufanya baada ya maseneta kujibu mapigo baada ya Bush kutoka kukutana nao Capitol Hill ili kuwanyamazisha na wasinyamaze.

Wakati sakata hilo likiendelea, vyombo vya habari vimegundua kuwa Marekani imeamu kuwasajili jeshini wasenge,wahalifu sugu wa zamani hata watoro wa shule ili kupata watu wa kwenda mstari wa mbele hasa nchini Afghanistan.

Hii ni baada ya nchi 34 zilizoombwa na Marekani kuchangia majeshi ili kuzima hujuma za watalebani zinazozidi kuongezeka kukataa kufanya hivyo wakihofia usalama wa majeshi yake.

Wakati nchi hizo zikikataa, baadhi ya washirika wa Marekani wanaanza kufikiri upya mantiki na madhara ya vita inayoendelea nchini Afghanistan hata Irak.

Kwani mshirika wa karibu wa Marekani yaani Canada, kwa sasa inapambana na upinzani mkubwa toka wananchi na vyama vya upinzani unaoongozwa na kiongozi wa upinzani Jack Layton.

Bw. Layton anasema wazi kuwa waziri mkuu wa Canada Bw. Stephen Harper anaonekana kuburuzwa na Bush.
Upinzani huu umetokea baada ya Canada kupoteza wanajeshi wengi mwaka huu kwenye mapigano huko Afghanistan.
Canada ilianza kuisaidia Marekani nchini humo tangu mwaka 2002.

Marekani kwa sasa inakabiliwa na hasara kubwa kutokana na vita nchini Afghanistan na Irak. Kwani kupitia kipindi cha Cafferty File kinachorushwa na CNN, takwimu zinafichua kuwa hadi sasa askari zaidi ya 2,000 wameishauawa katika Iraq na Afghanistan huku wengine zaidi ya 4,000 wakiwa wamepoteza viungo vyao.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  3. Is Tanzania a safe place to invest?
  4. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
  5. Nitaendelea kugombea nafasi za kisiasa- Balozi Karume
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Linda Garner
  4. Nthelezi Nesaa
  5. Marshy Abdu
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.