Safu hii mara nyingi hujadili mambo mbali mbali bila kuacha nyuma suala zima la dini na mila zetu. Leo pasina kupitwa na wakati tumejikita kwenye kuijadili alama mojawapo kuu na kongwe ya mojawapo ya dini mojawapo kongwe. Tutajitahidi kuonyesha chanzo hata upogo urongo unaozunguka uwepo,ujio,utumizi na maana nzima ya alama hii ya msalaba.
Kama ilivyo alama ya nyota na mwezi, msalaba ni alama kuu na muhimu ya dini ya kikristo. Msalaba ni sawa na bendera ya nchi kwa ukristo. Hivyo ni alama muhimu na yenye thamani kubwa. Je inastahiki kupata heshima na umuhimu huu ? Hilo ndilo swali kuu la kushughulika nalo leo.
Twende kazini. Ushahidi wa kwanza kuwa msalaba una chimbuko na maana kwenye dini za awali za kipagani unapatika kwenye katiba yenyewe ya ukristo yaani biblia wanayoiita wao takatifu. Soma waebrania 12 ;2 kwa ufafanuzi zaidi.
Pia kuonyesha ujio na uwepo wa msalaba na mkanganyiko wa jamii ya waumini inayoifuata biblia, waweza kusoma 1 wakorintho1 ;17 na 18 ambapo mitume wanatukuza tendo lililofanyika kwenye msalaba na siyo msalaba kama ilivyo sasa.
Kabla ya kwenda mbali lazima tukiri kuwa uchambuzi wetu utaonyesha jinsi msalaba ulivyokuwepo kama alama ya dini za kipagani hata kabla ya kuzaliwa kwa Yesu mwenyewe. Tutajaribu kufanya hivyo ili kuonyesha upagani ulivyopaganisha ukristo huku na ukristo ukikiristisha upagani na kufanya ndoa ya mashaka inayoendelea hadi leo tunaandika.
Katika kamusi ya Expository of new tastment words, yaani kamusi fafanuzi ya maneno ya agano jipya, inasema kuwa msalaba kama alama ya kipagani ilianzia kule Ukaldayo ( ambapo pia ndiko chimbuko la Ibrahimu). Kamusi hii inasema kuwa wapagani wa eneo hili waliitumia alama ya msalaba kama heshima yao kwa muungu wao wa kipagani aliyeitwa Tammuz ambaye kimsingi ni Nimrodi muwindaji na mwanzilishi wa himaya ya Babeli iliyolaaniwa kuliko hata firauni.
Tammuz kwa ufupi aliitwa « Tau » akitumia alama ya T kama alama yake kuu au sahihi tuseme. Alama hii ya T kama ishara ya Tammuz pia ilitumika si ukaldayo tu bali hata misri na asia wakati ule ikizingatiwa kuwa Tammuz aliweza kuabudia karibia maeneo hayo yote wakati wa himaya yake.
Msalaba pia unaweza kupatikana katika jamii za kimisri za kipagani za hapo mwanzo. Ushahidi huu unapatikana kule kwenye jengo la Amenopolis IV kule Tabes nchini misri. Msalaba huu unajulikana maarufu kama « Msalaba wa Misr au Msalaba wa tau. Hii ni kutokana na baadhi ya kazi za wanahistoria maarufu wa zama zile. Msalaba huu ulikuwa na mduara upande wa kichwani ukiashiria alama ya Tammuz akiwa kama muungu jua hapo baadaye.
Pia katika maeneo ya Ufoenike,China na Mexco inapatikana dhana nzima ya matumizi ya kidini ya msalaba kama alama yao kuu. Ikumbukwe kuwa yote hii ni kabla ya kuzaliwa kwa Yesu hivyo kabla ya ukristo tulio naos asa.
Jamiii nyingine unapopatikana msalaba kama alama shufaa ni maeneo kuanzia nchi ya Niger ya sasa hadi mto Nile. Kwani ngao za mashujaa wa eneo hili zilichorwa alama hii kama ishara ya utaua na ukuu.
Ushahidi madhubuti waweza kupatikana pia nchini Mexco ambako msalaba maarufu wa Palengue unapatikana. Kwa anayetaka ushahidi zaidi juu ya hili aweza kusoama kwenye “The catholic encyclopidia “ ambayo licha ya kuuita msalaba wa Palengue inauita msalaba wa kabla ya ukrist wa Palengue.
Msalaba huu nchini uliitwa pia Tota ama baba kama ambavyo baadaye uliitwa kwenye biblia. Soma Yeremia 2 ;27 hii imebainika kuwa upotofu mkubwa kuanzia lugha hata matumizi ya neno baba kumaanisha msalaba.
Nchini Misri inapatikana pia michoro ya au picha ya Muungu Amon akiwa ameshikilia msalaba wa Tau.
Pia kwenye hekalu la serapis kule Alexandria lilibeba alama ya msalaba.
Hata kwenye vita bain aya Alexander Mkuu (Alexander the great),na waajemi, waajemi walibeba msalaba kama alama yao ya ushindi. Pia hapa ikumbukwe kuwa utumizi wa alama ya msalaba kwenye vita ilianzishwa na akina Nebkadneza na wenzake kama alama ya ushindi.
Kwa ufupi angalau msomaji anaweza kuona utamaduni huu wa kuutukuza na kuutumia msalaba ulikotoka kuwa ni kwenye dini za kipagani za kale. Hiki ndicho tulichomaanisha tuliposema kuwa upagani umepaganisha ukristo na ukristo umekristisha upagani na kufanya ndoa kuu ya urongo na mashaka.
Hebu tuhame twende nchini Italia ambako ndiko chimbuko hasa la ukristo chini ya himaya ya kiroma. Mwaka 46 kabla ya kuzaliwa Yesu, kunapatikana sarafu za muungu jupiter zikiwa na alama ya msalaba ambao kwa wapagani wa kiitaliano ulitumika kama hirizi au sihiri kama unavyotumiwa na baadhi ya madhehebu ya kikristo kwa sasa.
Hata ukiangalia sarafu aliyoletewa Yesu alipe kodi ilikuwa na Maandishi Partem max yaani baba mkuu ambaye alikuwa ni kaizari, ilikuwa na alama ya msalaba. Hilo leo siyo mjadala wetu hivyo tutalitumia kwenye ushahidi huu tu.
Hata kule Ugiriki ulichorwa msalaba kwenye vibanio na nembo ukiwa ni alama ya mfalme wao aliyefanana sana na Tammuz.
Tusiwachoshe na rejea na ubukuzi na uchokonozi. Hebu tujiulize swali rahisi. Je msalaba hadi hapa ni alama ya Kimungu au kimiungu ? je inaingia akilini hadi leo mtu kuendelea kuutukuza na kuuvaa shingoni ikiwa ni kama kinga au hirizi kwake ? je kama mtu atategemea kulindwa na msalaba huyo Mungu atafanya kazi gani jamani !
Je inaingia akilini kuendelea kuutumia msalaba kwenye mahekalu ya Mungu,nyumba zetu,makaburi yetu,kuuchora kwenye vipaji vya uso kila mtu aingiapo kanisani na mengine kama hayo ? Je ni nani mwehu huyo awezaye kuivaa shingoni bastola iliyotumika kumuua mpendwa wake kama kinga ? kama hata akili nyepesi ingetumika basi bastola ingeogopewa kiasi cha kutisha kwani ndiyo iliyouchukua uhai wa mpendwa wako. Je ni nini mantiki ya wakristo kuvalishwa kongwa bila makosa ?
Je inaingia akilini kwa mtu ambaye amejua maana na chimbuko la msalaba kuendelea kuivaa hiyo kongwa na alama ya laana ? kazi kwenu. Je anayefanya hivyo anaendelea kuwa mkristo wa kweli au mpagani wa kawaida tu hata akijiita mkristo ?
Hatulengi kudhalilisha imani za wenzetu wala kuwaonyesha kama majuha lakini ni ujuha kutumia alama ya kipagani ambao kimsingi ndiye adui mkubwa wa dini. Tunaandika haya kwa kuzingatia ushauri wa bure lakini wa maana wa Yesu. Alisema kuwa mkiitafuta kweli itawawa huru kweli kweli. Kama hivyo ndivyo kwanini nasi tusiwaweke huru kweli kweli ?
Kwa taarifa yako msomaji msalaba umekuwa nongwa kwa wakatoliki hasa. Kwani huchora alama ya msalaba kila waingiapo kanisani,kunywa au kula,wakati wa kulala wakati wa kuamka n.k Pia msalaba huchorwa kwenye mwili wa mtu tangu siku ya kuzaliwa (kubatizwa) hadi kuzikwa huku kaburi lake likiubeba milele !
Kwa waroma msalaba uko kila mahali. Kwenye meza,makanisa,hata tumbo la kanisa limejengwa kwa ishara ya msalaba, hata kwenye vikombe wanavyotumia kanisani hufunikwa kwa kitambaa chenye alama ya msalaba. Kwa taarifa yako ni kwamba padre hufanya alama ya msalaba mara 16 wakati akiendesha misa huku akiongeza mara 30 za kuibariki altare!
Kama kweli msalaba ni alama ya laana na ya kipagani huku ni kufanya nini kama siyo kuwalaani waumini hata madhabahu yao . Je hapa kunaweza kuepukika kwa mabalaa na majanga yanayolikumba kanisa kama vile ulawiti na uzinzi wa mapadre wake?
Imekuwa ni jadi kw mkatoliki kujilaani kwa kila afanyalo. Hali wala hanywi bila kujitia alama hii ya laana.
Hata tukiambwa kuwa msalaba unatumiwa kama alama ya kusulubiwa kwa Yesu ambaye ni alama ya ukombozi wa kinjozi, bado haiingii akilini kwani zana na nyenzo hii ilianza kutumika kabla ya kuzaliwa na kusulubiwa kwake. Je ni wapi ukiachi siku ya kusulubiwa ulipoona Yesu na wanafunzi wake wakiongozana na msalaba kwenye shughuli zao za kueneza injili?
Tuhitimishe. Huko Misri, Ugiriki , Syria na Karthago,Palestina na Roma msalaba pia ulitumika kuwaadhibia wahalifu waliokuwa wametenda maovu makubwa kama alama ya kulaaniwa kwao.
Kimsingi msalaba na matumizi yake vimepotoshwa sana kama ilivyo kwa dhana kuu ya ubaba. Soma Matayo 23;9 hadi 11. tukiache magube ya kanisa ,hili liko wazi kuwa msalaba hauna uhusiano na ukristo wala dini aliyoileta Yesu. Huenda tukikubali kusema kuwa Ukristo siyo dini aliyoleta Yesu twaweza kuyakumbatia na kuyakubali matumizi ya msalaba kwa raha bila ubishi.
Lakini si kosa la kanisa. Kwani kama hadi leo halijamjua Yesu mwenyewe litajuaje upogo na najisi ya msalaba kwa kazi ya Mungu? someni Matayo 6 ;8, Matayo 10 ;34, Matayo 13 ;55 na 56 na Matayo 27 ;46,Marko 10 ;17 kwa ushahidi wa haraka na kwa ufupi ndipo utagundua upogo na magube yak anisa katika matumizi ya dhana mbali mbali.
Tuhitimishe kwa kukaribisha hoja juu ya kuyavinjari haya tunayoletewa bila kuhoji. Huu ndiyo wakati muafaka wa kuhoji na kuhoji na kuhoji hadi kweli ipatikane ili ituweke huru kweli kweli.