Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wasomi Chuo Kikuu waibana serikali
Wasomi Chuo Kikuu waibana serikali
By Habari Tanzania | Published  09/15/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Mkolo Kimenya

SERIKALI imetakiwa kuangalia upya uwezekano wa kutoa udhamini pamoja na mikopo kwa wanafunzi wa stashahada na shahada za juu katika vyuo vikuu nchini, ili iwe na uhakika wa kuwa na wataalamu wake watakaochangia kupunguza umasikini nchini.

Hayo yalielezwa jana katika Ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO), Dar es Salaam na wanafunzi wa stashahada na shahada za juu waliokosa udhamini katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam.

Udhamini huo hutolewa na Bodi ya Mikopo kwa wanafunzi wa vyuo vya elimu ya juu, lakini kwa sasa, ni wanafunzi wa stashahada na shahada ya kwanza ndio wanaonufaika na mikopo hiyo. Bodi, imetangaza kuondoa udhamini na mikopo kwa wanafunzi wa shahada za juu kuanzia mwaka wa masomo 2006/2007.

Katika taarifa yao iliyosomwa na Bilhuda Shirima kwa niaba ya kamati ya wanafunzi zaidi ya 130 walioingia katika mtego wa Bodi ya Mikopo, ilieleza kuwa suala la mikopo kwa wanafunzi hao linapaswa kuangaliwa upya, kwani linaweza kuleta athari kubwa kwa nchi katika siku za usoni.

Mbali ya kuelezea hofu ya kuminywa katika soko la ajira katika Jumuiya ya Afrika Mashariki inayokusudiwa kuundwa ikiunganisha nchi za Tanzania, Kenya na Uganda, wasomi hao pia walielezea hofu yao juu ya hatima ya elimu ya juu nchini.

“Ikumbukwe nchi jirani kupitia mifumo yao ya bodi za mikopo kwa wanafunzi zinasisitiza wanafunzi wa shahada za juu kukopa kwa lengo la kupata wataalamu wengi zaidi katika kada mbalimbali.

“Tanzania isipofuata mfumo huo, itaachwa nyuma na kitakachotokea ni kuona wataalamu wakiletwa kutoka nchi hizo na nyingine za nje kufanya kazi ambazo Watanzania wanaweza kuzifanya endapo watasomeshwa,” ilieleza sehemu ya taarifa hiyo.

Ulitolewa mfano wa tatizo la wawekezaji nchini kudai kukosa wataalamu ndani ya nchi pindi wanapokuja kuwekeza, hivyo kutumia mwanya huo kuajiri wataalamu kutoka nchi za nje.

Kuhusu hatima ya elimu ya juu katika siku za usoni, wasomi hao walielezea hofu ya vyuo vya Tanzania kutawaliwa na wahadhiri wageni, kwani Watanzania walio wengi watashindwa kustahili kwa kazi hiyo kutokana na kunyimwa fursa ya kusoma kwa kukosa mikopo au udhamini.

“Licha ya kufundisha katika vyuo vikuu, kwa kuandaliwa sasa, sisi na wengine wa stashahada na shahada za juu, tuna nafasi ya kuisaidia nchi katika programu kama za MKUKUTA, MKUKUZA na MKURABITA, kwani watalaamu wa fani mbalimbali, watafiti na kadhalika, watapatikana kwa kusoma.

“Dira ya Wizara ya Elimu ya Juu ni kuifanya Tanzania kuwa nchi yenye misingi imara ya kuifanya kuwa mshindani katika nyanja za elimu ya juu, sayansi na teknolojia. Pia dhima ya serikali ni kuwezesha upatikanaji wa nguvu kazi yenye uwezo wa kutumia rasilimali zilizopo ili kujiletea maendeleo.

“Je, serikali kupitia Wizara ya Elimu ya Juu ina maana wao hawalitambui hili? Au ni propaganda zinazoandikwa tu kwenye sera? Na kama wanalitambua, kwa nini wameondoa mikopo kwa ngazi za stahahada na shahada za juu? Au haitambui kama sisi ni rasilimiali inayotakiwa kuwezeshwa na kuendelezwa ili kusaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo?” ilihoji sehemu ya taarifa hiyo ya kurasa tano


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by balitazali)
    Rating
    Je, serikali kupitia Wizara ya Elimu ya Juu ina maana wao hawalitambui hili? Au ni propaganda zinazoandikwa tu kwenye sera? Na kama wanalitambua, kwa nini wameondoa mikopo kwa ngazi za stahahada na shahada za juu? Au haitambui kama sisi ni rasilimiali inayotakiwa kuwezeshwa na kuendelezwa ili kusaidia kusukuma mbele gurudumu la maendeleo?

    Hayo maswali hakuna asiye yajua hila ni magumu kujibika. Wanasiasa wanayajua hila hayawahusu kabisa. Watu hawawezi kuwekeza bila wataalamu.

    Jibu ambalo ni rahisi ni wafanye wajinga waweze kutawaliwa
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.