Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  TCC yajikwaa kibiashara
TCC yajikwaa kibiashara
By Habari Tanzania | Published  09/11/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

FAIDA iliyopata Kampuni ya Sigara Tanzania (TCC), baada ya kodi ilishuka kutoka sh bilioni 10 hadi sh bilioni 7.1 kwa kipindi kilichoishia Juni mwaka huu.

Taarifa ya kampuni hiyo iliyochapishwa kwenye magazeti mbalimbali juzi inaonyesha kuwa kushuka huko kwa faida ni sawa na asilimia 29.

Taarifa hiyo pia ilisema kuwa kampuni hiyo ilibidi ikope sh bilioni tatu ili kunusuru hali hiyo ya fedha ya kampuni.

Urari wa kampuni hiyo unaonyesha kuwa ulipungua kutoka sh bilioni 7.4 hadi sh bilioni moja.

Hali pia haikuwa nzuri kwenye gawio la awali, kwani lilishuka kutoka sh 78 hadi Juni mwaka jana; kwa hisa moja hadi sh 50 katika kipindi hicho kwa mwaka jana. Kushuka huko ni sawa na asilimia 35.

Wachambuzi wa mambo ya biashara wanasema kuwa ripoti hiyo ya fedha ya kampuni haitawafurahisha wanahisa wake.

Vyanzo vyetu vya habari ndani ya kampuni hiyo vinasema kuwa hali hii inasababishwa na gharama kubwa za uendeshaji na matangazo.
Sababu nyingine ni fedha nyingi kutumika kwenye promosheni na matangazo.

Pia wafanyakazi kadhaa wanalaumu pia matumizi yasiyo ya lazima kwa kuwalipa wataalamu wa kigeni kwa kazi ambazo zingefanywa na Watanzania.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.