- Aahidi kutafuta wafadhili kuisaidia Idara ya Upasuaji Bandia
- Ampandisha Ndege Bakari Kurudi Tabora
- Mtoto asema Mungu Atakubariki
IKULU
09.09.2006
DAR ES SALAAM
Rais Jakaya Kikwete ameushukuru uongozi wa Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, hususani Profesa Atef Amin na Dk. Laurean Rwanyuma kwa kufanikisha upasuaji na matibabu yaliyomrejesha katika hali yake ya kawaida mtoto Bakari Hamisi Katumbaku.
Kutokana na furaha yake hiyo, na kuridhishwa na kazi kubwa inayofanywa na madaktari katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Rais ameuagiza uongozi wa hospitali hiyo, kufanya utafiti wa kina wa gharama za baadhi ya mashine muhimu zizonahitajika katika Idara ya upasuaji bandia(plastic Surgery) ili awatafute watu wenye mapenzi mema wagharamie mashine hizo.
Alitoa shukrani hizo na agizo hilo, jana jioni wakati alipomkaribisha mtoto Bakari Hamisi Katumbaku Ikulu kwa lengo la kumujilia hali na kuagana naye baada ya kukamilika kwa matibabu yake. Mtoto huyo alifika Ikulu akifuatana na Mama yake, Bi Aziza Hamisi Katumbaku, Daktari wake, Laurean Rwanyuma na Muuguzi, Bi Ritha Kitama. Profesa Atef Amin ambaye ni rais wa Misri hakuweza kufika kutoka na majukumu hospitali hapo.
Mara Rais alipomuona mtoto Bakari akitembea vizuri kabisa bila dalili zozote za kujikuja au maumivu kama alivyomwona mara ya kwanza kule Sikonge.
Alitamka “ nashukuru sana, umepona kabisa, daktari nashukuru sana, nilipomwona mara yakwanza Sikonge, hali yake ilikuwa mbaya, alikuwa akitembea kwa kuinama na akajitahidi kunikimbilia kama watoto wenzie lakini kwa tabu sana. Nikasema mungu akijalia nitakusaidia, Mungu Mkubwa, nimefurahi sana”.
Akaongeza “ Nawashakuru sana, ehe, angalia, Bw. Bakari, sasa mambo safi sasa, unatembea kama watoto wenzio, sasa huna mawazo wala uchungu tena, utakuwa na raha sasa umerudi katika hali ya kawaida, sasa kasome kweli kweli , ili uje kumsaidi mama, na sisi tutakuwa tunafuatilia maendeleo yako shuleni akasema rais. Na kuachia tabasamu pana.
“ Daktari hebu kafenye tathimini halisi ya ghara za mashine mnazosema zinahitajika sana.Niliteeni gharama halisi za mashine hizo, wapo watu wenye mapenzi mema wanaotaka kupata thawabu kwa Mwenyezi Mungu, watakuwa tayari kugharamia mashine hizo ”alisisitiza rais.
Akitoa shukrani zake kwa Rais, mtoto Bakari ambaye alikumbatiana kwa furaha na Rais kama Baba na Mwana, alisema “Nakushuru sana, Rais, Mungu Akujalie, sina cha kusema nakushuru sana. Nimefurahi sana.
Naye Mama wa Bakari yeye alikuwa na haya ya kusema. “ Nakushukuru sana, na kukupongeza kwa kutimiza ahadi yako, haikuwa rahisi kwangu kuamini pale nilipoletewa taarifa kwamba Umeaagiza tuje muhimbili kwa matibabu. Sikutegemea kama mtoto wangu leo angeweza kutembea vizuri kama watoto wenzie. Nakushukuru sana Mhe. Rais”.
Katika maelezo yake kwa Rais kuhusu upasuaji aliyofanyiwa mtoto Bakari aliyeungua moto wakati akiwa na umri wa miaka sita na kumsababisha maumivu makali yaliyomfanya ashindwe kutembea vizuri, alisema, idara ya upasuaji katika hospitali hiyo, haina mashine muhimu ambazo zingesaidia sana kuokoa maisha ya Watanzania wengi hususani wale wanaopata ajali za kuungua moto na kupoteza asilimia kubwa ya ngozi zao.
Dk Rwanyuma alisema idara hiyo ambayo hadi miaka ya hivi karibuni ilikuwa haina wataalamu wa upasuaji bandia, isipokuwa wale wakutoka nchini misri inahitaji mashine zinazoweza kuotesha ngozi au kuitanua hususani pale mgonjwa anapokuwa amepoteza asilimia zaidi ya 80 ya ngozi yake na hivyo kubakiwa na ngozi kidogo tu ambayo haiwezi kutosha kufunika majeraha yake yote.
Aidha alisema kuwa pamoja na kupatikana kwa mashine hizo, pia mafunzo yanahitajika ili kuweza kupata wataalamu wengi zaidi katika idara hiyo, hali aliyosema itasaidia sana katika si tu kuokoa maisha ya watanzania bali pia kurekebisha viungo vyao na kuwafanya watu wenye furaha.
Rais alisema ni vizuri mashine hiyo ikapatikana ili maisha ya watanzania wengi zaidi yaweze kuokolewa. Na hivyo kusisitiza apewe maelezo kamili ya aina na gharama za mashine hizo.
Rais Kikwete alimweleza daktari huyo kwamba vifaa vya uchunguzi ni muhimu sana na hususani katika hospitali kubwa kama Muhimbili “ wenzetu Ulaya wanatushinda kwa sababu wanavifaa na mitambo ya uchunguzi, kwahiyo nasisi lazima tujielekeze katika kuiwezesha hospitali yetu kupata mashine na mitambo muhimu ya uchunguzi. Lazima na sisi tukimbizane na teknolojia mpya huo ndio uwe moyo wetu. Ili tuweze kuokoa maisha ya watanzania wengi”.
Katika kukamilisha furaha yake, Rais aliwaagiza maafisa wake, kuhakikisha kwamba wanampatia usafiri wa ndege, mtoto Bakari na Mama yake, katika safari yake ya kurudi nyumbani.
Mwisho.