Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wajane ‘wamvamia’ mke wa Rais
Wajane ‘wamvamia’ mke wa Rais
By Habari Tanzania | Published  09/8/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu, Zanzibar

WANAWAKE wafanyabiashara ya bidhaa za utalii katika eneo la Forodhani mjini Zanzibar, wameandamana hadi ofisi za mke wa Rais wa Zanzibar, Shadya Karume, wakipinga kuporwa mali zao kulikofanywa na Baraza la Manispaa.

Wafanyabiashara hao 25 walisema kwamba bidhaa zilizoibwa ni za thamani kubwa.

Wakizungumza na waandishi wa habari mjini Zanzibar jana, walisema kwamba askari waliwavamia na kukamata bidhaa zao kwa madai ya kuendesha biashara eneo lisiloruhusiwa.

“Sisi tangu mwaka 1990 tumekuwa tukifanya biashara katika eneo la Forodhani na tunalipa kodi ya sh 15,000 kila mwezi, kwa nini tufukuzwe

na kuporwa bidhaa wakati pale ndipo tunapopatia maisha?” alihoji Tatu Ahmada.

Walisema kwamba kitendo hicho kinakwenda kinyume cha kauli ya serikali ya kuwataka kina mama wajiajiri ili waondokane na umaskini.

Walieleza kwamba baada ya kutokea tukio hilo waliamua kwenda kuonana na Mama Karume, lakini walikwama baada ya kuzuiwa na wasaidizi wake.

“Tulipofika ofisini kwake, wasaidizi wake wametwambia suala hilo halimhusu na kututaka tumtafute Mkuu wa Mkoa wa Mjini Magharibi ili aweze kulishughulikia,” alisema mmoja wa kina mama hao.

Mkurugenzi wa Baraza la Manispaa Zanzibar, Mabrouk Jabu, alithibitisha kukamatwa kwa kina mama hao, na alisema madai ya kuporwa mali zao, linahitaji uchunguzi.

Alisema Baraza la Manispaa Zanzibar linaendesha operesheni ya kuwaondoa wavamizi katika maeneo yasiyoruhusiwa kuendesha biashara.

Alieleza kwamba wafanyabiashara wote ambao wanaendesha biashara katika maeneo yasiyoruhusiwa, watahamishiwa katika eneo jipya la Saatanei baada ya ujenzi wake kukamilika. Hakusema lini ujenzi huo utakamilika.

Tangu juzi, mji wa Zanzibar, askari wa Manispaa wamekuwa wakifukuzana na wafanyabiashara wadogo wadogo na kubomoa vibanda vyao. Miongoni mwa maeneo yaliyokwisha kufikiwa ni Mji Mkongwe na Michenzani.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments
  • Comment #1 (Posted by Hamis Nsombo)
    Unrated
    Ili kuweka jiji la Zazibar katika hali ya usafi mpangilio wa sehemu ya kufanyia biashara ni suala la kuzingatia changamoto kubwa kwa mkurugenzi ni kuhakikisha maeneo yaliyotengwa kwa ajili ya wafanyabiashara yanakuwa tayari kabla kuwahamisha
     
Submit Comment


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.