RAIS Jakaya Kikwete amemteua, Daniel Yona, kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Utalii nchini katika kipindi cha miaka mitatu ijayo. Uteuzi huo umeanza Agosti 15 mwaka huu.
Taarifa kwa umma iliyotolewa jana na Wizara ya Maliasili na Utalii, inaeleza kuwa sambamba na uteuzi huo, Waziri wa wizara hiyo, Anthony Diallo, amewateua wajumbe watano watakaounda bodi hiyo.
Wajumbe hao ni Tully Mwambapa (Meneja Masoko wa Benki ya CRDB), Raymond Mrope (Mbunge wa Masasi), Profesa Raphael Mwalyosi (Mbunge wa Ludewa), Malima Lubeleje (Mbunge wa Mpwapwa) na Mohamed Nathani (Mwenyekiti wa Shirikisho la Utalii Tanzania).
Diallo amewateua wajumbe hao kwa mujibu wa sheria namba 18 (1992), iliyoanzish Bodi ya Utalii nchini.