Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  TSJ waunga mkono serikali
TSJ waunga mkono serikali
By Habari Tanzania | Published  09/4/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Edmund Mihale

BODI ya Wakurugenzi ya Chuo cha Uandishi wa Habari cha Time, Dar es Salaam, imesema inaunga mkono kauli ya serikali ya kuunda chombo kitakachoangalia ubora wa kazi za wandishi wa habari na vyombo wanavyofanyia kazi.

Akizungumuza katika hafla ya kuwakaribisha wanafunzi wapya chuoni hapo, mmoja wa wakurugenzi wa bodi hiyo, Maurice Maugo, alisema uamuzi huo utaleta ufanisi kwenye taaluma hiyo.

“Sisi tunaunga mkono suala hili kwani itafanya taaluma hii iwe na ubora unaotakiwa, tunakitaka chombo hicho kuwa makini katika kufanya ukaguzi na kwenye vyuo vinavyotoa taaluma hiyo.

“Tunataka watembelee vyuo vyote vidogo na vikubwa, lakini wasitoe hukumu ya kufanana kwa sababu vingine haviko kwenye ngazi ya vyuo vikuu, vikaguliwe kwa kiwango chao,” alisema Maugo.

Hata hivyo, aliitaka serikali kuweka mtaala mmoja kwenye vyuo vinavyotoa mafunzo ya taaluma hiyo ili kupata ubora wa wanataaluma hiyo.

“Ili kuepusha tofauti iliyopo kati ya chuo kimoja na kingine, serikali ikubali kutumia rasilimali zake kuhakikisha kuwa kinatunga mtihani wa aina moja katika vyuo vyote vya uandishi wa habari,” alisema.

Chuo hicho kilianzishwa mwaka 2000 na kinatoa elimu ya uandishi wa habari katika ngazi ya cheti na diploma.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.