Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Syria yaigeuka Hezbollah
Syria yaigeuka Hezbollah
By Habari Tanzania | Published  09/3/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
DAMASCUS, Syria

KATIBU Mkuu wa Umoja wa Mataifa (UN), Koffi Anan, alisema kwamba Syria itaweka jeshi la doria mpakani na kushirikiana na jeshi la Lebanon kuzuia uvushaji wa silaha kwa kundi la Hezbollah.

“Syria itaongeza jeshi lake la doria kwenye mpaka wa Lebanon na Syria na kuuunda jeshi la pamoja na Lebanon ikiwezekana,” Anan alisema baada ya kukutana na Rais wa Syria Bashar Assad mjini hapa juzi.

Assad hakutoa kauli yoyote hadharani baada ya mkutano huo, lakini Anan alizungumza na waandishi wa habari kwenye uwanja wa ndege mjini hapa kabla ya kuondoka kuelekea Qatar.

Azimio la UN lililomaliza mapigano kati ya Israel na Hezbollah linataka kuwekewa vikwazo kwa wapiganaji hao wa msituni, na Lebanon kulinda mipaka yake na sehemu nyingine za kuingilia.

Anan alisema Assad amemfahamisha kwamba Syria itachukua hatua madhubuti kutekeleza aya ya 15 ya azimio la UN namba 1701, linalozitaka nchi zisiuze au kugawa silaha kwa vikundi nchini Lebanon bila kibali cha Serikali ya Lebanon au walinda amani wa UN.

Pia Anan aliitaka Syria itumie ushawishi wake ili kuachiwa kwa askari watatu wa Israel, wawili wakiwa wametekwa na Hezbollah Julai 12 wakati wa mapigano ya mpakani yaliyosababisha vita na mmoja akiwa ametekwa na wanamgambo wanaohisiwa kuwa wa Hamas huko Gaza miezi michache iliyopita.

Assad alisema kwamba anaunga mkono kuachiwa kwao, lakini pia alitaka kuachiwa kwa wafungwa wa Syria wanaoshikiliwa Israel, Anan alisema.

Anan alitarajia kutembelea Iran jana ambako miongoni mwa mambo atakayolenga ni programu ya nyuklia ya nchi hiyo na suala la vita Mashariki ya Kati.

AP


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.