Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kiingilio Stars, Burkina Faso chapoa
Kiingilio Stars, Burkina Faso chapoa
By Habari Tanzania | Published  08/31/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
na Deodatus Mkuchu

SHIRIKISHO la Soka Tanzania (TFF), limepunguza kiingilio cha mechi ya kimataifa kati ya timu ya soka ya Tanzania, Taifa Stars dhidi ya Burkina Faso itakayofanyika Jumamosi kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Taarifa ya TFF iliyotolewa jana na kusainiwa na rais wake, Leodegar Chilla Tenga, punguzo hilo limehusu kiingilio cha mzunguuko ambako itakuwa ni sh 2,000 badala ya sh 3,000.

Punguzo hilo limekuja siku moja baada ya wapenzi na mashabiki wa soka kulalamika mbele ya Rais Jakaya Kikwete juzi kuwa, kiingilio ni kikubwa.

Hata hivyo, punguzo hilo limehusu mzunguko tu kwani viti maalumu itakuwa ni sh 20,000, jukwaa kubwa sh 10,000 na kijani ni sh 6,000.

Juzi, Rais Kikwete alifika katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume ulioko Ilala, Dar es Salaam na kushuhudia mazoezi ya timu hiyo kabla ya kuzungumza na wachezaji.

TFF imempongeza Rais Kikwete kwa kusema, ameonyesha ni jinsi gani alivyo na uchungu wa maendeleo ya soka na kwamba, amechochea hamasa kwa wachezaji na Watanzania kwa ujumla.

Aidha, kambi ya Stars jana ilihama kutoka Karume yaliko makao makuu ya TFF hadi Hoteli ya Regency Park iliyoko Msasani na Burkina Faso, wanatarajiwa kuingia leo saa 11:00 jioni.

Stars Jumamosi itacheza mechi ya kwanza dhidi ya Burkina Faso ikiwa ni mwanzo wa kampeni ya kusaka tiketi ya kucheza fainali za Mataifa Afrika mwaka 2008.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.