MASHABIKI kadhaa wa soka wameahidi kufurika kwenye Uwanja wa Taifa keshokutwa ili kuishangilia timu ya taifa, Taifa Stars itakayokwaana na Burkina Faso katika mchezo wa awali kuwania kucheza fainali za Mataifa ya Afrika huko Ghana 2008.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti juzi kwenye Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, Ilala jijini Dar es Salaam, mashabiki wengi wameonyesha kutiwa moyo na ziara ya ghafla ya Rais Jakaya Kikwete aliyoifanya juzi.
Mmoja wa mashabiki hao, Jumanne Mbaraka aliyejitambulisha kwamba ni mfanyabiashara sokoni Kariakoo, alisema kwamba ana matumaini Stars itashinda kwa jinsi inavyojiandaa chini ya Kocha Mkuu, Mbrazil Marcio Maximo.
Mdau mwingine, Emmanuel Eliwedi aliyejitambulisha Mhandisi Mwandamizi wa Kampuni ya ME & Co. Ltd ya Mikocheni jijini Dar es Salaam, alisema kwamba licha ya timu hiyo kuwa chini ya Maximo kwa kipindi kifupi, lakini kwa jinsi ilivyojinoa, ana imani