Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Lowasa kuzuru Thailand, Vietnam
Lowasa kuzuru Thailand, Vietnam
By Habari Tanzania | Published  08/31/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

WAZIRI Mkuu, Edward Lowassa, anaondoka nchini leo kwenda Thailand na Vietnam kwa ziara rasmi ya kikazi kwa mwaliko wa mawaziri wakuu na nchi hizo.

Madhumuni ya ziara hiyo ni kupanua ushirikiano wa Tanzania na nchi hizo; kisiasa, kiuchumi na kijamii na kupata uzoefu wa nchi hizo wa kurekebisha uchumi kwa muda mfupi.

Akiwa Thailand, atazuru viwanda vinavyoshughulika na madini, hasa ukataji na usafishaji wa vito na miradi ya kuondoa umasikini, na uanzishwaji wa benki ya wanawake.

Waziri Mkuu atafuatana na Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha; Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko, Nazir Karamagi; Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto, Dk. Batilda Burian.

Septemba 4, Waziri Mkuu atakapoondoka Thailand, Dk. Msabaha atabaki kufuatilia masuala ya madini na Dk. Burian atabaki kujifunza shughuli za akiba na mikopo kwa ajili ya uanzishwaji wa benki ya wanawake.

Akiwa Vietnam, Waziri Mkuu, amepangiwa kukutana na wafanyabiashara aweze kuwashawishi kuwekeza katika kilimo cha umwagiliaji na viwanda vya kusindika mazao.

Atafanya pia ziara katika Chuo cha Sayansi ya Kilimo na kuzuru mashamba ya kahawa na korosho na viwanda vya kusindika mazao hayo.

Nchini Vietnam, Waziri Mkuu atafuatana na mkewe, Mama Regina Lowassa; Waziri wa Kilimo na Chakula, Joseph Mungai; Waziri wa Kilimo na Mazingira Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Burhan S. Haji.

Wengine ni Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Dk. Christine Ishengoma; Mkuu wa Mkoa wa Mbeya, John Mwakipesile; Mbunge wa Iramba Magharibi, Mgana Msindai (CCM) na Magdalena Sakaya (CUF, Viti Malum, Tabora).

Wengine ni Balozi Mteule wa Tanzania nchini China, Vietnam na Cambodia, Ramadhan Mapuri; Mkurugenzi wa Idara ya Asia na Australia, Balozi Nguma.

Waziri Mkuu na ujumbe wake wanatarajia kurejea nchini Septemba 10, mwaka huu


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.