Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Majambazi wateka basi na kupora abiria
Majambazi wateka basi na kupora abiria
By Habari Tanzania | Published  08/28/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Watu wanaodhaniwa kuwa majambazi, wakiwa na bunduki aina ya shotgun, wameliteka gari dogo la abiria aina ya Hiace lililokuwa likitokea Horohoro kwenda Tanga mjini na kuwapora fedha abiria Sh. 190,000 na dola 600 za Kimarekani.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tanga, Bw Issaya Mngulu, alisema tukio hilo lilitokea mwishoni mwa wiki saa 1:30 usiku katika eneo la Magaoni Mzambarauni baada ya majambazi hayo kuweka gogo kubwa kwenye daraja.

”Hiace iliyokuwa ikitokea Horohoro ilikuta gogo katika daraja eneo la Magaoni Mzambarauni lililowekwa na majambazi waliokuwa kati ya watatu au watano ambao baada ya kusimama, waliwateka abiria kwa kuwatisha na bunduki ya shotgun na kuwapora fedha zao,” alisema Kamanda Mngulu.

Alisema mmoja wa abiria hao Bw. Salim Hussein (32), aliibiwa Sh. 190,000 na dola 600 za Kimarekani, simu na vitu vingine vidogo vidogo ambavyo walipora kutoka kwa abiria.

Hata hivyo, alisema watu wawili wanashikiliwa na polisi kuhusiana na tukio hilo.

Katika hatua nyingine, Kamanda Mngulu amesema mvulana mwenye umri wa miaka 15, (jina limehifadhiwa), anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa Shule ya Msingi Stahabu wilayani Pangani mwenye umri wa miaka 16 (jina limeahifadhiwa).

Alisema tukio hilo lilitokea Agosti 23, mwaka huu huko katika kijiji cha Stahabu wilayani Pangani mkoani hapa saa 5:00 usiku ambapo mvulana huyo alimuingilia kwa nguvu mwanafunzi huyo baada ya kumkuta nyumbani kwao amelala.

Hata hivyo, Kamanda Mngulu alisema wanafanya uchunguzi wa kina kuhusiana na madai hayo ili waweze kumfikisha mtuhumiwa mahakamani.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.