Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Raza adaiwa kuongopa Zanzibar
Raza adaiwa kuongopa Zanzibar
By Habari Tanzania | Published  08/25/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

UONGOZI wa Hospitali ya Mnazi Mmoja, Zanzibar umesema taarifa zilizoripotiwa na vyombo vya habari nchini kwamba umekataa msaada wa mfanyabiashara Mohamed Raza, ni za uongo.

Akizungumza na waandishi wa habari katika Hoteli ya Ngurdoto mkoani hapa, Mkurugenzi wa Afya na Ustawi wa Jamii wa Hospitali hiyo, Dk. Juma Sadala, alisema kilichoelezwa na Raza hakina ukweli.

Alisema msaada wa Raza haukukataliwa, bali walitofautiana katika maudhui.

“Raza alitaka kutoa msaada wa magodoro na vitanda, hakuwasiliana na uongozi kufahamu nini hasa kipaumbele cha hospitali hiyo kwa sasa, ukweli unabaki pale pale kwamba hatukukataa msaada,” alisema Dk. Sadala.

Aliongeza: “Haiwezekani mtu akatoa msaada bila kutuuliza aina ya msaada tunaouhitaji.”

Alisema baada ya kumweleza hivyo, Raza alikwenda kwenye vyombo vya habari kulalamika.

Alitoa mfano kwamba kuna wakati mfanyabiashara huyo alitoa msaada wa glovu zikiwa pungufu ya ahadi aliyotoa.

Dk. Sadala alisema kwa sasa wanahitaji msaada wa kukarabati maabara na paa la Mnazi Mmoja. Kazi zote zinagharimu kiasi cha sh milioni 30.

Alisema wasingekubali vitanda kwa vile tayari vipo.

Kauli hii inagongana na iliyotolewa na Raza, akishutumu kukataliwa kwa msaada aliopanga kuipa Hospitali ya Mnazi Mmoja.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.