Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Watetea matumizi ya dawa za ARV’s
Watetea matumizi ya dawa za ARV’s
By Habari Tanzania | Published  08/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Deogratius Temba, SAUT

KATIBU wa Chama cha Waishio na Virusi vya UKIMWI na Matumaini (CHAWAVUMA), Mkoa wa Kilimanjaro, Dickson Malle, amesema dawa za kuongeza muda wa kuishi kwa waathirika wa UKIMWI (ARV’s), hazina madhara kama mtumiaji atafuata masharti.

Akizungumza na Tanzania Daima Dar es Salaam mwishoni mwa wiki, Malle alisema kumekuwapo madai na taarifa kuwa dawa hizo zinawadhuru watumiaji.

Alisema dawa hizo ni nzuri, na zinawasaidia watumiaji, lakini huwa na madhara pindi mtumiaji anapokiuka masharti.

“Tumesikia malalamiko hayo, tulifanya utafiti wetu kwa watu tunaowafahamu ambao wanazitumia, tukagundua walioathirika ni wale wasiofuata masharti.

“Dawa hizi ni kali, zinahitaji mtumiaji apate lishe nzuri na afuate masharti-kila siku akiamka, anatakiwa anywe, na asiache hata siku moja mpaka siku anakufa.

“Masharti mengine ya hizi dawa kwa mwathirika, anapaswa kuacha kufanya ngono, kunywa pombe, kuvuta sigara, kufanya kazi nzito au mazoezi mazito,” alisema Malle.

Alisema kuwa kama mwathirika atafuata masharti hayo na kupata mlo safi, dawa hizo hazitamsababishia madhara.

Naye Meneja wa Mtandao wa Mashirika yanayopiga vita UKIMWI mkoani Kilimanjaro (KINSHAI), Veronica Shayo, alisema dawa hizo zinasaidia, isipokuwa watumiaji wengi wanakiuka masharti.

Alisema kuwa kama dawa zitatumika vizuri na kufuata lishe bora, waathirika wataishi vizuri.

“Inaonekana watu wengi wanaotumia na kupata matatizo ni wale wenye shida ya chakula,” alisema.

Tume ya Taifa ya Kupambana na UKIMWI (TACAIDS), imeshakanusha madai ya kwamba dawa hizo ni hatari kwa watumiaji.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.