Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Waziri Mwandosya apongeza mipango ya Mazingira ya wilaya ya Kibondo
Waziri Mwandosya apongeza mipango ya Mazingira ya wilaya ya Kibondo
By Habari Tanzania | Published  08/21/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Na. Prosper Kwigize

Kibondo

Wilaya ya Kibondo imepongezwa kwa jitihada zake za kulinda, kutunza na kuboresha mazingira zinazoshirikisha ngazi zote za serikali za vijiji, watu binafsi na asasi zisizo za kiserikali.

Pongezi hizo zimetolewa leo na waziri wa nchi ofisi ya makamu wa Rais anayeshughulikia mazingira Bw. Mark Mwandosya wakati akizungumza na viongozi wa wilaya baada ya kupokea taarifa ya wilaya iliyosomwa kwake na mkuu wa wilaya luteni Kanal John Mzurikwao.

Amesema taifa liko katika changamoto nyingi za kuhakikisha mazingira yanalindwa na kutunzwa kikamilifu bila kuathiri shughuli za kijamii na kuongeza kuwa wananchi wanahitaji sasa kuhamasishwa.

Mheshimiwa Mwandosya amesema mikakati iliyowekwa na wilaya hiyo ya kuwashirikisha wananchi kwa kutunga sheria ndogondogo za vijiji ni nzuri na inasitahili kuwa darasa kwa wilaya nyingine nchini.

Hata hivyo waziri Mwandosya ameulaumu mkoa wa Kigoma kwa kukithiri katika uchomaji moto horela katika mapori na kuongeza kuwa pamoja na juhudi za kupambana nalo ipo haja ya kuongeza kasi zaidi.

Ameelezea kusikitishwa na kitendo cha kupokelewa na moshi wa moto uliokuwa ukiwaka katika mapori yliyoko kandokando ya barabara kuu itokayo Kigoma hadi wilayani Kibondo.

Waziri wa nchi ofisi ya makamu wa rais anayeshughulikia mazingira profesa Mark Mwandosya yuko wilayani Kibondo kwa ziara ya siku mbili kukagua shughuli za mazingira.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.