Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Msichana jasiri azidi kusaidiwa
Msichana jasiri azidi kusaidiwa
By Habari Tanzania | Published  08/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wetu, Monduli

MFANYABIASHARA maarufu nchini, Jacqueline Noni, amemchangia mwanafunzi wa kidato cha kwanza, Tausi Ibrahim (17), sh 200,000 baada ya kusoma habari zake.

Tausi anasoma Shule ya Sekondari ya Manyara wilayani Monduli, Arusha.

Noni, alisema mwishoni mwa wiki kwamba ameguswa mno na msichana huyo baada ya kusoma habari za kujitokeza kwake mbele ya Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na kueleza matatizo ya ada yanayomsibu.

Tausi, alijitokeza kwenye mkutano wa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na kueleza shida yake ya ada, na kisha Askofu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya mkoani Arusha, Thomas Laizer, aliahidi kanisa kumsomesha hadi ukomo wa elimu yake.

Noni alisema baada ya msaada huo, msichana huyo sasa anapaswa afunguliwe akaunti ili wasamaria wema wamwekee fedha za kumsaidia.

“Namshukuru na kumpongeza Baba Askofu kwa msaada wa kumlipia ada, sasa walio karibu inabidi wamfungulie akaunti ili aweze kusaidiwa zaidi.

“Mimi naahidi kumsaidia sh 200,000, ingekuwa rahisi zaidi kwake kuzipokea kama angekuwa na akaunti, nawaomba walio karibu naye wamfungulie akaunti mapema,” alisema.

Noni alisema fedha hizo zitamsaidia Tausi katika matumizi na mahitaji mengine, hasa ikizingatiwa kuwa yeye kama msichana, ana mahitaji muhimu.

Tausi, akitokwa machozi, alimweleza Lowassa kwamba anakabiliwa na matatizo makubwa ya ukosefu wa ada.

“Nimehangaika sana kwa kukosa ada…sina baba (alishakufa) na mama yangu ni kilema, hawezi kuhangaika, niliposikia unakuja nikalazimika kutoroka shule kwa sababu mwalimu alininyima ruhusa ya kuja huku,” alisema Tausi huku akilia


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.