Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Matapeli waliza wananchi Mnazi Mmoja D’Salaam
Matapeli waliza wananchi Mnazi Mmoja D’Salaam
By Habari Tanzania | Published  08/19/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mussa Ngarango

KAMPUNI hewa ambayo inajitambulisha kuwa inahusika na mashamba ya ufugaji mbuni mkoani Arusha, inadaiwa kuendesha vitendo vya utapeli jijini Dar es Salaam kwa kutumia jina la Rais Jakaya Kikwete na la Waziri wa Maendeleo ya Mifugo, Dk. Shukuru Kawambwa.

Mmoja watu walioonja chungu ya kutapeliwa, alisema kwamba, matapeli hao wameweka makazi yao ya muda katika viwanja vya Mnazi Mmoja. Jina hewa la kampuni hiyo kwa sasa tunalihifadhi.

Wanaendesha vitendo vya kitapeli kwa kuwafanyia usaili baadhi ya watu wenye kusumbuliwa na tatizo la ajira.

“Wanamsimamisha kila mtu anayepita eneo hilo, ukisimama wanakuuliza kama una shida ya ajira - wewe binafsi au ndugu yako - hawajali kiwango chako cha elimu, kwa kuwa asilimia kubwa ya watu hawana ajira huwakubalia, baada ya usaili hutakiwa walipe sh 5,000 halafu hutaka mhusika asubiri matokeo, humpa stakabadhi,” alisema mmoja wa waathirika.

Watu hao hudai kwamba watu watakaochaguliwa, kabla ya kupelekwa Arusha kwenye mashamba hayo, watakutana na Dk. Kawambwa ili awape utaratibu.

Watuhumiwa hao wanadai wana baraka kutoka kwa Rais Kikwete, na kwamba mara kwa mara huenda Ikulu kwa wito wa Rais ambaye anawachukulia kama wakombozi wa ahadi zake za kutoa ajira.

Juzi mwandishi wa habari hizi alifika Mnazi Mmoja na kukutana na mmoja wa matapeli hao, ambao ni nadhifu.

“Wote mnaohitaji kufanya usaili nisubirini nitakuja baada ya muda mfupi, nimeitwa Ikulu na Rais Kikwete mara moja nadhani tutaonana baada ya nusu saa,” ndivyo alivyoelezwa mwandishi wetu pamoja na wote waliokuwa wakisubiri kufanyiwa usaili.

Hata hivyo tapeli huyo hakutokea hadi baada ya saa tatu wakati baadhi ya watu walipoanza kukata tamaa ya kufanyiwa usaili.

Baadaye ilitolewa kauli kwamba ‘ofisa’ huyo alikuwa katika mazungumzo marefu na Rais ambaye alikuwa akijiandaa kwenda Lesotho; na akawataka waonane baada ya siku mbili.

Katika hali ya kusataajabisha, wengi walioibiwa sh 5,000 kutokana na usaili huo, walionekana kuamini maneno ya matapeli hao.

Tanzania Daima ilikwenda kwa Msajili wa Kampuni kujua kama kweli kuna kampuni yenye jina hilo iliyosajiliwa kufanya kile inachofanya.

Hapakuwapo na jina la kampuni hiyo wala taarifa nyingine za kuthibitisha kile wanachofanya.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.