Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  TMK Wanaume kuanzia Dar
TMK Wanaume kuanzia Dar
By Habari Tanzania | Published  08/18/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
na Ruhazi Ruhazi

KUNDI la muziki wa kizazi kipya, TMK Wanaume Family, limebadili ratiba ya uzinduzi wa albamu tatu za pamoja na wasanii Juma Kassim ‘Sir Nature’, Amani Abbas Temba ‘Mh Temba’ na Rashid Ziada ‘KR Mullar’.

Akizungumza na mwandishi wa habari hizi jana, Meneja wa kundi hilo, Saidi Fella, alisema kwamba uzinduzi huo sasa utaanzia jijini Dar es Salaam Septemba 8, mwaka huu badala ya Septemba 15 ya awali.

Alisema kwamba mabadiliko hayo yametokana na Ukumbi wa PTA waliopanga kufanyia uzinduzi Septemba 15 kutumika kwa kazi nyingine na hivyo wamelazimika kurudisha nyuma kwa wiki moja.

“Tumebadili ratiba yetu ya uzinduzi, hivyo sasa tutaanzia Dar es Salaam badala ya Arusha, tutazindua Septemba 8 na Septemba 9, kama kawaida tutazindua Tripple A jijini Arusha, na Septemba 19 tutazindua Mwanza. Mchana tutakuwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba na usiku tutazindua kwenye Ukumbi wa Capri Cabana,” alisema.

Fella alisema kwamba mbali ya kuzindua, pia watauza mavazi na viatu vyenye nembo ya kundi hilo kwa bei ya kawaida ili mashabiki wao waweze kununua.

Sir Nature anazindua albamu ya nne iitwayo ‘Zote Historia’, wakati Mh Temba anazindua albamu ya pili aliyoipa jina ‘Ipo Siku’ na KR Mullar anazindua albamu yake ya kwanza iitwayo ‘Kamua kwa Uwezo’ zilizoko sokoni.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.