Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wadau wa UKIMWI hawana takwimu’
Wadau wa UKIMWI hawana takwimu’
By Habari Tanzania | Published  08/18/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Ahmed Makongo, Bunda

WADAU wengi wa mapambano dhidi ya UKIMWI wamekuwa wakipanga mipango yao kiholela na bila kuwa na viashiria vya kuaminika, kwa kuwa hawana taarifa sahihi za maambukizi.

Hayo yameelezwa juzi mjini hapa na Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika lisilo la kiserikali la Afnet, Sara Mwanga kwenye warsha ya mtazamo mpya kuhusu janga la UKIMWI Tanzania.

Alisema kuwa kufanyika kwa utafiti wa HIV/AIDS Indicators Survey (HIS), uliofanyika mwaka 2003/2004, umeleta sura mpya na kuondoa utata uliokukwapo ambapo sasa kuna takwimu sahihi na za uhakika katika mapambano dhidi ya UKIMWI.

Alisema kuwa kwa kutambua tatizo hilo USAID ilitoa msaada kwa mradi wa Policy Project na kuandaa kitabu kinachoelezea takwimu za UKIMWI kwa lugha nyepesi na kwamba Afnet ilishiriki katika maandalizi ya kitabu hicho kiitwacho ‘Mtazamo mpya kuhusu janga la UKIMWI Tanzania’ ambacho kilichapwa na Tume ya Taifa ya Kudhibiti UKIMWI.

Hata hivyo, alisema kuwa pamoja na vitabu hivyo kusambazwa katika wilaya zote nchini, lakini watu hawavisomi ipasavyo na kwamba, wadau wengi hawana habari juu ya takwimu hizo na wanaendelea kuandika miradi na programu kwa kutumia takwimu zisizo sahihi na ambazo hazijathibitishwa.

Mratibu wa Afnet Mkoa wa Dodoma, Andrew Karama, alisema warsha hiyo ni miongoni mwa warsha zinazoendeshwa na shirika hilo pamoja na mtandao wa wanawake wanaoishi na virusi vya UKIMWI kwa kushirikiana na Health Policy Initiative chini ya ufadhili wa USAID, ili kujenga ufahamu zaidi juu ya takwimu zilizo katika utafiti wa HIS


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.