Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wakamatwa wakidaiwa kutapeli waomba viza
Wakamatwa wakidaiwa kutapeli waomba viza
By Habari Tanzania | Published  08/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Magreth Kinabo

JESHI la Polisi Mkoa wa Kinondoni, limewakamata watuhumiwa wawili wa utapeli wa kuwatafutia watu viza katika balozi mbalimbali nchini.

Akizungumza na Tanzania Daima ofisini kwake jana, Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Kinondoni, Jamal Rwambow, alisema: “Sisi tumechunguza ili kugundua kundi la watu wanaojihusisha na kitendo cha kujipatia fedha kwa udanganyifu wa kuwatafutia viza watu katika balozi mbalimbali.”

Alisema Agosti 11, mwaka huu, walimkamata John Bitebo (45), mkazi wa Magomeni Mwembechai, akiwa na ndani ya gari lenye namba T 907, aina ya Toyota Mark II.

Alisema baada ya kufanya upekuzi kwenye gari hilo, walimkuta akiwa na viza tano za watu mbalimbali Watanzania ambazo alishindwa kuzitolea maelezo.

Baadaye mtuhumiwa huyo alimtaja anayeshirikiana naye, aliyefahamika kwa jina la Ally Salum (46), mkazi wa Tegeta, Dar es Salaam.

Alisema watu hao juzi walifikishwa katika Mahakama ya Kisutu wakati upepelezi ukiendelea. Kesi hiyo itatajwa Agosti 30, mwaka huu.

Agosti 3, mwaka huu gazeti hili lilitagaza kupotea kwa viza mbili za wafanyakazi wa New Life Foundation zilizotolewa Dar es Salaam.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.