Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Kipindupindu chazidi kuenea Dar
Kipindupindu chazidi kuenea Dar
By Habari Tanzania | Published  08/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Dauson Harold

WATU 17 wanaoumwa kipindupindu wamelazwa katika Manispaa ya Kinondoni na Temeke, Dar es Salaam.

Taarifa iliyotolewa na Mganga Mkuu wa Jiji la Dar es Salaam, Dk. Deo Mtasiwa, ilisema kuwa wagonjwa wapya tisa walilazwa jana katika hospitali mbalimbali mkoani humo.

Wagonjwa wanne walitoka katika Manispaa ya Kinondoni, na wengine walitoka katika Manispaa ya Temeke. Manispaa ya Ilala haikuwa na mgonjwa.

Aliwataka wananchi wachemshe maji ya kunywa, ya kuoshea vyombo, na ya kutengenezea juisi ili kuepuka kuenea kwa ugonjwa huo.

Alipiga marufuku kutiririsha maji machafu mitaani, kuuza vyakula kiholela na kutupa taka hovyo.

Alisema wote watakaokiuka kanuni za afya, watachukuliwa hatua za kisheria.

Kipindupindu ni ugonjwa unaoenezwa na nzi, chanzo kikuu kikiwa ni uchafu na kwa kutozingatia kanuni za afya.

Dalili za mgonjwa wa kipindupindu ni kuhara kinyesi cha majimaji chenye rangi inayofanana na ya maji yanayotokana na mchele uliooshwa, kutapika na kupoteza nguvu.

Wataalamu wanashauri kuwa pindi dalili hizo zinapoonekana, ni vema mgonjwa akapewa huduma ya kwanza.

Inashauriwa mtu wa aina hiyo apewe maji mengi yaliyotiwa chumvi au sukari, kisha apelekwe haraka katika zahanati, kituo cha afya au hospitali iliyo karibu.

Ugonjwa wa kipindupindu ni hatari, na huambukiza haraka na kwa njia rahisi. Inashauriwa mgonjwa atengewe eneo maalumu ili asiwaambukize watu wengine


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.