Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mama ajifungua watoto 3 kwa mpigo akiwa nyumbani
Mama ajifungua watoto 3 kwa mpigo akiwa nyumbani
By Habari Tanzania | Published  08/16/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Thomas Kiani, Singida

MKAZI wa kijiji cha Musimi kata ya Sepuka Singida vijijini, Bibi Habiba Shabani amejifungua watoto wa watatu kike watatu kwa mpigo.

Kwa mujibu wa habari kutoka kwa mama huyo aliyesaidiwa na mkunga wa jadi Bibi Mwajuma Choyo, zilisema huo uzazi wa tatu kwake.

”Mara ya kwanza nilijifungua mtoto wa kiume, mara ya pili wa kiume, safari hii watatu wa kike kwa mara moja,” alisema.

Katika watoto hao watatu, wa kwanza alizaliwa akiwa na uzito wa kilo 2.1, wa pili kilo 2.02 na wa mwisho kilo mbili.

Mwenyekiti wa Mtaa wa Italala anamoishi mzazi huyo, Bw. Shabani Gunda, alisema mama huyo alijifungulia nyumbani salama watoto wote watatu Julai 21 mwaka huu na baadaye kupelekwa kituo cha afya cha Sepuka kwa uchunguzi zaidi ya afya yake na watoto wake.

Maelezo kutoka kituo hicho cha Sepuka yalieleza kwamba mama na wanawe walikuwa na afya nzuri.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Musimi, Bw. Jumanne Njoghomi, ambaye alikwenda kuwajulia hali watoto na mama yao mzazi na kumpongeza, alisema haijawahi kutokea tukio la namna hiyo la kuzaliwa watoto watatu kwa mara moja tena wa kike katika kijiji chake na hata vijiji vya jirani.

Alimsifu baba wa watoto hao, Bw. Ramadhani Makiya, kwa kuwa mvumilivu muda wote wa ujauzito wa mkewe na kumtakia heri na hekima katika kuwalea watoto hao inavyotakiwa.

Kwa mila na desturi za kinyaturu kabila la familia hiyo, inahesabiwa kwamba ni tukio la kishujaa kwa wazazi wote hivyo wazee na makungwi hutakiwa kujumuika pamoja na kufanya sherehe siku nzima.

Pia hutoa maombi maalumu ya kuwatakia heri na fanaka katika malezi ya watoto hao.

Wazazi wa mapacha hao waliiomba Serikali na jamii na asasi zote kuwasaidia katika malezi ya watoto hao kwa sababu hawana uwezo wa kimapato

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.