Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wabunge walaani filamu
Wabunge walaani filamu
By Habari Tanzania | Published  08/7/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Wabunge wa mkoa wa Mwanza wanaungana na wananchi wa mkoa wa Mwanza walioandamana kuonyesha imani yao, mshikamano na kuunga mkono hotuba ya Rais Jakaya Kikwete, aliyoitoa mwisho wa mwezi wa Julai ikilaani maudhui ya filamu ya ”The Darwins Nightmare”.

Wabunge hao walitoa kauli hiyo mwishoni mwa wiki walipokutana kujadili hotuba ya Rais kuhusu filamu ya The Darwins ambayo wamedai kuwa ilikuwa na lengo la kushusha uchumi wa mkoa wa Mwanza.

Walisema waliipokea hotuba ya Rais kwa furaha wakati anaongea na wananchi wa mkoa wa Mwanza hususani alipotoa kauli yake ya kulaani na kukanusha maudhui ya filamu hiyo ambayo ilitengenezwa na matayarishaji wa kigeni Bw. Hubert Sauper, mwaka jana na kuwashirikisha Watanzania wachache katika filamu hiyo.

Aidha, wabunge hao walisema wakiwa kama wawakilishi wa wananchi wa mkoa wa Mwanza, hawakubali kamwe nchi ichezewe na kudhalilishwa na wageni wasioitakia mema nchi yao.

Walisema kuwa mkoa wa Mwanza umejaliwa rasilimali nyingi kama madini, ziwa, samaki, mifugo na mazao mbalimbali ya chakula na biashara ambapo walisema inawezekana mtayarishaji wa filamu hiyo alikuwa na lengo la kuvuruga uchumi wa mkoa wa Mwanza.

Walisema wanahisi mtayarishaji wa filamu hiyo ana mpango wa kuvuruga uchumi hasa katika biashara ya samaki ambayo ndio tegemeo kubwa la uchumi katika mkoa wa Mwanza.

Aidha, walisema kama wabunge wa mkoa wa Mwanza, hawatakubali kuona uchumi wa mkoa wao unavurugwa na wanaungana na wananchi wa mkoa wao kulaani filamu hiyo.

Wabunge hao walisema wananchi wa Mwanza wataendelea kuvua, kushiriki katika biashara na uzushi wa Bw. Saupre hautawarudisha nyuma wananchi wa Mwanza.

Walioomba serikali kumchukulia hatua za kisheria mtu huyo na kumpiga marufuku kuingia nchini

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.