Shule ya Msingi Nengo iliyopo wilayani Kibondo mkoani Kigoma inakabiliwa na uhaba wa samani, nyumba za walimu pamoja na vyumba vya madarasa
Mwl. mkuu wa shule hiyo Benedict Nkundwa amesema kuwa shule yake inakabiliwa na uhaba wa madawati 86 hali inayochangia kutumia dawati moja wanafunzi watano na wengine kukaa chini
Pia amesema shule ya msingi Nengo inakabiliwa na uhaba wa vyumba sita vya madarasa hivyo kuwa na msongamano wa wanafunzi wengi kwani darasa moja hutumiwa na wanafunzi sitini hadi sabibini badala ya 45.
Kadharika Mwl Nkundwa amelitaja tatizo lingine linaloikabili shule hiyo kuwa ni uhaba wa nyumba za walimu, na kueleza kuwa shule hiyo ina nyumba sita za walimu wakati hitaji ni nyumba 21, na walimu wengine hulazoimika kupanga mtaani.
Aidha Mwl Nkundwa amesema Ili kuondokana na matatizo hayo ameomba jamii kuhamasishwa juu ya kuchangia gharama za elimu pia akaiomba serikali kutuma fedha za MMEM mapema ili ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa katika kipindi Muafaka.
Hata hivyo ulichunguzi wa mwandishi wa habari hii unabaini kuwa matatizo ya upungufu wa samani na nyumba za walimu ni wa shule zote wilayani Kibondo licha ya shule kupata ufadhili wa mfuko wa maendeleo ya elimu MMEM kwa ajili ya kukomesha mapungufu hayo.