Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Shule za msingi Kibondo zakabiriwa na uhaba wa vitendea kazi
Shule za msingi Kibondo zakabiriwa na uhaba wa vitendea kazi
By Prosper Kwigize | Published  07/26/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Mwandishi Wa HabariTanzania.com, Kibondo
Shule ya Msingi Nengo iliyopo wilayani Kibondo mkoani Kigoma inakabiliwa na uhaba wa samani, nyumba za walimu pamoja na vyumba vya madarasa
 
 Mwl. mkuu wa shule hiyo Benedict Nkundwa amesema kuwa shule yake inakabiliwa na uhaba wa madawati 86 hali inayochangia kutumia dawati moja wanafunzi watano na wengine kukaa chini
 
 Pia amesema shule ya msingi Nengo inakabiliwa na uhaba wa vyumba sita vya madarasa hivyo kuwa na msongamano wa wanafunzi wengi kwani darasa moja hutumiwa na wanafunzi sitini hadi sabibini badala ya 45.
 
 Kadharika Mwl Nkundwa amelitaja tatizo lingine linaloikabili shule hiyo kuwa ni uhaba wa nyumba za walimu, na kueleza kuwa shule hiyo ina nyumba sita za walimu wakati hitaji ni nyumba 21, na walimu wengine hulazoimika kupanga mtaani.
 
 Aidha Mwl Nkundwa amesema Ili kuondokana na matatizo hayo ameomba jamii kuhamasishwa juu ya kuchangia gharama za elimu pia akaiomba serikali kutuma fedha za MMEM mapema ili ziweze kufanya kazi iliyokusudiwa katika kipindi Muafaka.
 
 Hata hivyo ulichunguzi wa mwandishi wa habari hii unabaini kuwa matatizo ya upungufu wa samani na nyumba za walimu ni wa shule zote wilayani Kibondo licha ya shule kupata ufadhili wa mfuko wa maendeleo ya elimu MMEM kwa ajili ya kukomesha mapungufu hayo.
 

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.