Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Siku ya Mashujaa yafana Dar
Siku ya Mashujaa yafana Dar
By Habari Tanzania | Published  07/26/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Shabani Matutu

MAMIA ya wananchi jijini Dar es Salaam, jana walijitokeza katika viwanja vya Mnazi Mmoja, kushuhudia maadhimisho ya Siku ya Kumbukumbu ya Mashujaa waliopigana vita kwa ajili ya kutetea uhuru wa taifa hili.

Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume, ndiye aliyekuwa mgeni rasmi katika maadhimisho hayo.

Rais huyo alikuwa mgeni rasmi kutokana na Rais Jakaya Kikwete kuwa ziarani nchini Ujerumani, Waziri Mkuu, Edward Lowassa kuwa bungeni mjini Dodoma wakati Makamu wa Rais, Dk. Mohamed Shein, yupo nchini Uingereza kwa matibabu.

Rais Karume alianza kwa kuweka mkuki na mshale katika mnara wa mashujaa kama ishara ya silaha za jadi zilizokuwa zikitumika wakati wa vita ya ukombozi.

Naye Mkuu wa Majeshi, George Waitara aliweka sime katika mnara huo, Mwenyekiti wa chama cha Askari Wastaafu (Tanzania Legion), naye aliweka shoka.

Balozi wa Libya nchini, Bashiri Bashiri alifuata kwa kuweka shada la maua kama ishara ya kumbukumbu kwa mashujaa waliokufa, Mstahiki Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Adam Kimbisa pia alipata fursa ya kuweka upinde na mshale.

Katika kumbukumbu hiyo, askari walipiga mizinga miwili kama heshima na kumbukumbu kwa mashujaa waliokufa kwa ajili ya kuhakikisha Tanzania inakuwa huru.

Baadhi ya viongozi waliohudhuria ni pamoja na Jaji Mkuu wa Tanzania, Barnabas Samatta; Naibu Waziri Kiongozi wa Zanzibar, Ali Juma Shamuhuna; Rais mstaafu Benjamin Mkapa; Spika wa Bunge wa zamani, Pius Msekwa, Katibu Mkuu wa CCM, Yusufu Makamba; Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba na viongozi wa dini.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.