Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  ‘Wapiganaji’ wa Mrema wajiunga na Mbowe
‘Wapiganaji’ wa Mrema wajiunga na Mbowe
By Habari Tanzania | Published  07/26/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Giliard Sauli, IJMC

WANACHAMA watano wa chama cha Tanzania Labour Party (TLP), kinachoongozwa na Augustine Mrema, wamejiunga na Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kinachoongozwa na Freeman Mbowe.

Kaimu Katibu Mwenezi wa CHADEMA, Singo Benson aliwataja wapiganaji hao kuwa ni Walles Mkhoma, John Tendwa na Nicholas Mwakatobe.

Mwakatobe alikuwa mpishi wa Mrema tangu kiongozi huyo alipokuwa akiongoza chama cha NCCR-Mageuzi wakati Tendwa na Walles walikuwa walinzi wa kutumainiwa na Mrema, hasa kipindi cha kampeni za uchaguzi wa mwaka jana ambapo Mrema alikuwa mmoja wa wagombea wa urais.

Hata hivyo, Benson hakuwa tayari kutaja majina ya wanachama wengine wawili wa TLP waliohamia CHADEMA kwa madai kuwa wanaandaliwa hafla maalum ya kutangazwa rasmi.

Alisema wanachama hao wamehamia CHADEMA kwa madai kuwa chama chao (TLP), kinazidi kushuka umaarufu, hasa kutokana na migogoro ya mara kwa mara ndani ya chama hicho


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.