Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wawili wafariki katika ajali
Wawili wafariki katika ajali
By Habari Tanzania | Published  07/24/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Na Giliard Sauli, IJMC

WATU wawili wamefariki dunia juzi na wengine kumi na saba wamejeruhiwa katika ajali ya basi lenye namba za usajili T. 826 AHK, lililomgonga mwendesha baiskeli kabla ya kupinduka na kumuua utingo, Ibrahimu Kibwana.

Kaimu Kamanda wa Polisi  wa Mkoa wa Ilala, Masendoki Masendoki, amewaambia waandishi wa habari jana kuwa, ajali hiyo ilitokea saa saba na nusu  mchana maeneo ya Kigogo Fresh, Wilaya ya  Ilala.

Kaimu Kamanda huyo alisema kuwa basi hilo lilikuwa linatokea jijini Dar es Salaam kuelekea Kisarawe, Pwani na lilipofika maeneo ya Pugu Kajiungeni ndipo lilipomgonga David Benson (20) aliyekuwa akiendesha baiskeli.

 Masendoki alisema watu kumi na saba walijeruhiwa katika ajali hiyo, na   kukimbizwa katika Hospitali ya Wilaya ya Kisarawe kwa ajili ya matibabu.

 Hata hivyo wanane  kati yao waliruhusiwa baada ya kupatiwa matibabu na wengine saba waliojeruhiwa vibaya wanaendela na matibabu.

Aliwataja waliolazwa kuwa ni Miliza Bwake (30), Aishi Ally (20), Hadida Juma (12) na Ruth Mlaki (30). Wengine ni Shaaban Rajabu (30), Salima Pampe (30) na Sauda Moshi (18).

Katika tukio jingine, jeshi hilo linawashikilia watu sita kwa tuhuma za  kukamatwa na puli mbili  na kete 200 za bangi.

Kaimu Kamanda wa Polisi wa Temeke, Emmanuel Kandihabi, alisema kuwa watu hao walikamatwa baada ya jeshi hilo kufanya doria maeneo ya Yombo Vituka.

Wanaoshikiliwa ni Abasi Salum (23), Said Alfan (25) na Shabani Ulimwengu (28). Wengine ni Juma Khatib (22), Kangresi Charles (25) na Mashuku Dasai (26).


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.