Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Wavuvi watishia kupigana na mwekezaji
Wavuvi watishia kupigana na mwekezaji
By Habari Tanzania | Published  07/24/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Kulwa Karedia

KUNA hatari ya kuibuka mapigano makali baina ya wavuvi wa visiwa vya Bongoyo, Mbiji na Pangane  na  mwekezaji kutoka nchini Italia, kwa madai kuwa mwekezaji huyo anawanyanyasa kwa kuwakataza wasivue kwenye visiwa hivyo.

Mwenyekiti wa Chama cha Wavuvi Wadogo Wadogo Msasani (CHAWAWAM), Mohamed Tana, aliiambia Tanzania Daima  mwishoni mwa wiki kuwa, manyanyaso wanayopata kutoka kwa mwekezaji huyo yamefikia hatua mbaya.

“Sisi sasa tumechoshwa na  vitendo vya kunyanyaswa na mwekezaji huyo, kama serikali haitaingilia kati hapa kunaweza kutokea mapigano baina ya wavuvi na mwekezaji huyu…tumechoshwa jamani tukimbilie wapi?” alisema Tana.

Alisema mwekezaji huyo anawakataza wasivue samaki katika visiwa  hivyo akidai kuwa serikali imempatia yeye pekee kufanya kazi hiyo.

“Sisi tuna familia  na watoto wanatutegemea kutokana na kazi yetu hii, sasa tunapozuiwa na mwekezaji  huyo hatujui nini hatima yetu, ”alisema Tana.

Alisema licha ya kuzuiwa kuvua samaki katika eneo hilo, wavuvi wengi wamekuwa wakinyang’anywa zana zao za uvuvi kama  vyavu, mitumbwi na  walinzi wa mwekezaji huyo huku wakipigwa bila sababu.

Alisema miongoni mwa wavuvi waliopigwa mwishoni mwa wiki ni pamoja na Mussa Ali, Ndoga Mohamed Mussa, Hamis Abdallah na Mwindadi Msemwa.

Katika hatua nyingine, mwenyekiti huyo alisema kumeibuka mgogoro mkubwa katika soko la samaki Msasani kwa baadhi ya watu wajanja kutaka kulibinafsisha soko hilo bila kushirikisha viongozi wa soko hilo.

 Alisema mbinu za kuuzwa kwa soko hilo zimekuwa zikifanywa na mmoja wa viongozi wa kata hiyo, jina limehifadhiwa.

Uongozi wa chama hicho umeitaka serikali kuchukua hatua za haraka dhidi ya kiongozi huyo ambaye wanasema kwa  kipindi kirefu sasa amegoma kuidhinisha katiba ya chama hicho ambayo Tanzania Daima imepata nakala yake ili iweze kutambulika rasmi.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.