Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Mbarali wapambana na uhaba wa madawati
Mbarali wapambana na uhaba wa madawati
By Habari Tanzania | Published  05/19/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Solomon Mwansele, Mbarali
 
UHABA mkubwa wa madawati uliokuwa ukiikabili shule ya msingi Mahango Ruiwa iliyopo wilayani Mbarali na kusababisha wanafunzi wa darasa la tatu kukaa chini sasa umepatiwa ufumbuzi kufuatia madawati mapya 20 kutengenezwa.
 
Taarifa za shule hiyo kukumbwa na upungufu wa walimu wanane na madawati 57 uliopelekea wanafunzi hao kusomea chini ziliripotiwa na gazeti hili miezi miwili iliyopita.
 
Ilielezwa kuwa hali hiyo ya wanafunzi hao kukaa chini ilichangiwa zaidi na shule hiyo kuandikisha wanafunzi wengi waliojiunga na darasa la kwanza mwaka huu.
 
Akiongea na mwandishi wa habari hii Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Samwel Sheshambo, alisema madawati hayo 20 yametengenezwa na serikali ya kijiji cha Mahango Ruiwa kufuatia michango iliyotolewa na wananchi wa kijiji hicho.
 
Sheshambo alisema madawati mengine (hakutaja idadi), yamefanyiwa ukarabati na pia wamebuni utaratibu wa muda kwa wanafunzi wanne kukaa katika dawati moja wakati juhudi za kukamilisha madawati mengine 27 yanayohitajika zikiendelea kufanywa.
 
"Hadi sasa hakuna mwanafunzi anayekaa chini na madawati hayo mengine 27 yanayohitajika yatakuwa tayari yametengenezwa kufikia mwishoni mwa mwezi Juni, mwaka huu," alisema Sheshambo.
 
Kuhusu upungufu wa walimu shuleni hapo, Sheshambo alisema tatizo hilo nalo limeanza kupatiwa ufumbuzi kufuatia Ofisa Elimu wa wilaya hiyo kuwaongezea mwalimu mmoja na hivyo kufanya walimu waliopo shuleni hapo kufikia 7.
 
Alibainisha kuwa ofisa elimu huyo ameahidi kuwaongezea walimu wengine wanaohitajika ili kuondokana na upungufu wa walimu wanane hadi sasa unaoikabili shule hiyo.
 
Shule ya msingi Mahango Ruiwa yenye wanafunzi 530 na walimu 6 ilikuwa inakabiliwa na upungufu mkubwa wa madawati 57 kufuatia kuandikisha wanafunzi wengi waliojiunga na darasa la kwanza mwaka huu.
 
Katika shule hiyo kulikuwa na upungufu wa walimu wanane hali iliyopelekea walimu sita waliokuwepo kufanya kazi zaidi ili kuziba pengo hilo la upungufu wa walimu hao waliokuwa wanahitajika.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.