Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
By Habari Tanzania | Published  05/9/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Nyumba ya ghorofa moja iliyopo Karikoo Jijini katikati ya mitaa ya Kongo, Ndovu na Rufiji nusura liungue kwa moto.

Watu walioshuhudia moto huo wamesema chokochoko zilianzia kwenye ghorofa ya chini ya jengo hilo.

Wamesema chanzo cha moto huo ambao ulizimwa na Kikosi cha Kuzima Moto cha Jiji kabla haujaleta madhara ni hitilafu ya umeme.

Wakazi wa maeneo jirani na nyumba hiyo wamesema kama moto huo usingedhibitiwa mapema, ungeweza kuleta kasheshe kubwa kutokana na eneo hilo kuwa na majengo mengi na kuwa lenye heka heka nyingi za biashara.

Sababu nyingine iliyowafanya watu hao kuwa na hofu kubwa ni jirani na jengo hilo kuwa na ghala la kuuzia mkaa.

’Ni hatari sana kuuza mkaa karibu na makazi ya watu, kama moto usingedhibitiwa mapema ungeweza kuleta madhara makubwa,’ mmoja wa watu walioshuhudia amesema.

Habari zaidi kutoka kwenye tukio zinasema moto huo umesababisha uharibifu wa vifaa mbalimbali vilivyoko ndani ya jengo hilo ikiwa ni pamoja na kiyoyozi.
  • SOURCE: Alasiri

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Salehe Mmoro
  8. Ramadhan Semtawa
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.