Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Walemavu washirikishwe - Mbunge
Walemavu washirikishwe - Mbunge
By Habari Tanzania | Published  07/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Tamali Vullu, Dodoma

MBUNGE wa Viti Maalumu, Margareth Mkanga (CCM), ameitaka serikali kueleza ni kwa kiasi gani imewashirikisha watu wenye ulemavu katika ushiriki wa nchi katika mchakato unaoendelea kimataifa kuandaa mkataba wa haki za watu wenye ulemavu.

Mbunge huyo pia amehoji kama serikali ina habari juu ya mchakato huo.

Akijibu maswali hayo bungeni mjini hapa jana, Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Profesa David Mwakyusa, alisema kuwa, serikali inayo habari kuhusu mchakato wa mkataba wa kimataifa kuhusu haki za watu wenye ulemavu.

“Kamati ya Umoja wa Mataifa ilianza kukutana mwaka 2002 na imeendelea kukutana mara moja au mbili kila mwaka. Kikao cha karibuni kilifanyika Februari mwaka huu mjini New York ambapo nchi yetu iliwakilishwa na ubalozi wetu uliopo New York.

“Vikao hivi ni muhimu, na serikali inapaswa kuhudhuria, ili kuchangia maoni yetu katika mchakato mzima kwa niaba ya wananchi wetu wenye ulemavu. Kutokana na ukosefu wa fedha, serikali haijapeleka ujumbe kwenye vikao hivi,” alisema.

Waziri alisema  katika kikao cha mwisho cha mchakato huu na ambacho kitatoa maamuzi kuhusu mkataba kitakachofanyika Agosti mwaka huu, serikali inakusudia kutuma ujumbe.

Alisema ana imani kuwa ujumbe wa Tanzania kwenye mkutano huo utashirikisha watu wenye ulemavu.

Profesa Mwakyusa alisema matayarisho yamekamilika kwa Tanzania kuridhia kanuni hizo


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.