Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Serikali yasaka walioficha mafuta
Serikali yasaka walioficha mafuta
By Habari Tanzania | Published  07/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Tamali Vullu, Dodoma

SERIKALI imeanza msako rasmi dhidi ya wafanyabiashara wa mafuta ambao wanadaiwa kuyaficha kwenye maghala na kufanya bei ya nishati hiyo iwe ya juu.

Waziri wa Nishati na Madini, Dk. Ibrahim Msabaha, alisema hayo bungeni jana alipokuwa akielezea matatizo mbalimbali ya nishati nchini.

Hata hivyo, katika kauli yake hiyo, Msabaha hakusema ni adhabu ipi hasa watapewa wale watakaokutwa wameficha mafuta hayo.

“Hivi ninavyozungumza hapa bungeni, tayari serikali imetuma timu ya watu wake kwenda kwenye maghala ya wafanyabiashara ambao tumepata taarifa kwamba wameyaficha mafuta ya taa,” alisema.

Dk. Msabaha alisema lengo la kuyaficha mafuta hayo ni kufanya yawe kidogo kuliko mahitaji kwenye soko na hivyo bei ipande.

“Hii ni tamaa tu ya wafanyabiashara kutaka kupata faida, na serikali haiwezi kuwaachia waendelee na mtindo wao huo,” alisema.

Wakati akifanya majumuisho ya hotuba ya bajeti ya wizara yake aliyoiwasilisha mwanzoni mwa wiki, Dk. Msabaha alitangaza vita dhidi ya wafanyabiashara ya mafuta wenye tamaa ya kujitajirisha.

Alitangaza kwamba serikali imeamua kuliruhusu Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kuagiza mafuta ili kupunguza upandaji holela wa bei ya nishati hiyo.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.