Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Dk. Shein alazwa
Dk. Shein alazwa
By Habari Tanzania | Published  07/21/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

MAKAMU wa Rais, Dk. Ali Mohamed Shein, yuko London, Uingereza akipatiwa matibabu ya figo na kufanyiwa uchunguzi wa kawaida wa afya yake.

Taarifa iliyotolewa na ofisi yake jijini Dar es Salaam jana, ilisema Dk. Shein anatibiwa katika Hospitali ya London.

Mwandishi wa Habari wa Makamu wa Rais, Penzi Nyamunguni, alisema pamoja na kufanyiwa uchunguzi wa kawaida wa afya yake, Dk. Shein pia atapewa matibabu ili kuondoa vijiwe katika figo zake.

Alisema Oktoba, 2004, wakati akifanyiwa uchunguzi wa afya yake, alibainika kuwa na vijiwe hivyo.

“Kwa wakati huo, ilishauriwa kwamba hakukuwa na haraka ya kufanya matibabu hayo, wataalamu walishauri kuwa yanaweza kufanyika kwa siku za baadaye.

“Sasa imeonekana ni wakati mzuri akafanyiwa matibabu ili kuondoa vijiwe hivyo,” alisema Penzi.

Dk. Shein alifika London akitoka Brazil ambako alimwakilisha Rais Jakaya Kikwete katika mkutano wa kimataifa.

Penzi alisema: “Hali ya Mheshimiwa Makamu wa Rais inaendelea vizuri, anatarajia kurejea nyumbani wakati wowote.”


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.