Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Karume: Sifikirii kugombea urais 2010
Karume: Sifikirii kugombea urais 2010
By Habari Tanzania | Published  07/19/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
BALOZI wa Tanzania nchini Ujerumani, Bw. Ali Abeid Karume, amesema hana mpango wowote wa kuwania urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2010.
 
 Taarifa yake ya faksi kwa gazeti hili jana, ilisema maelezo yaliyotolewa na gazeti hili Julai mosi mwaka huu kuhusu kufikiria kugombea tena baada ya kuchujwa mwaka jana na CCM, hayakuwa na ukweli.
 
 "Sijawahi kusema au kutamka kwa mwandishi wenu au yeyote wa habari, kwamba nafikiria kugombea urais tena...maelezo hayo ya uongo na uzushi yanaweza kuleta mtafaruku baina yangu na Rais wa Tanzania na kuhatarisha ajira yangu serikalini," alilalamika Bw. Karume.
 
 Bw. Karume ambaye anakiri habari hizo pia kuandikwa na gazeti la Mtanzania amesisitiza kuwa hajafikiria bado kuwania kiti hicho cha juu nchini.
 
 Balozi Karume mwaka jana alikuwa mmoja wa wanachama 11 wa CCM waliojitokeza kuwania kugombea urais, lakini hatimaye chama hicho kikawachuja na kubakia Bw. Jakaya Kikwete, ambaye hatimaye aliibuka mshindi na kuwa Rais wa Serikali ya Awamu ya Nne.

Source: Majira

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.