Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Vibanda vinavyoonyesha picha za video vyabomolewa
Vibanda vinavyoonyesha picha za video vyabomolewa
By Habari Tanzania | Published  07/19/2006 | Habari za Kitaifa | Rating:
Vibanda vinavyoonyesha picha za video vyabomolewa
 
Na Stan Likomawagi, Morogoro
 
HALMASHAURI ya manispaa ya Morogoro imeanza kubomoa vibanda vinavyoonyesha picha za video kwa kutoza watu fedha katika maeneo mbalimbali nyakati za usiku.
 
Mkurugenzi wa halmashauri ya manispaa hiyo, Rafael Ndunguru, alisema shughuli hiyo imeanza katika maeneo mbalimbali kutokana na vibanda vingi kuonyesha picha za ngono hasa nyakati za usiku.
 
Alisema wapo watu wengi wanaonyesha picha za ngono kwenye vibanda vyao kwa kuwatoza watu sh. 50 kwa mtoto na watu wazima sh. 100.
 
Aliongeza kuwa hali hiyo ni hatari kwa kuwa hata watoto wadogo wanaingia katika vibanda hivyo na kujifunza vitendo vinavyochochea maambukizi ya ukimwi.
 
Ndunguru alisema mpaka sasa tayari amemkamata mkazi wa Chamwino na kumfikisha kituo cha polisi. Alidai mtu huyo ambaye amejenga kabisa banda lake amekuwa na tabia ya muda mrefu ya kuonyesha picha za ngono.
 
"Yule kijana nilimkamata juzi lakini wakati nampeleka polisi akaruka kwenye gari leo (jana) tumefanikiwa kumkamata na naagiza wakazi wa Morogoro waache kabisa tabia hiyo,"alisema Ndunguru.
 
Mkurugenzi huyo alisema tayari amevunja zaidi ya vibanda vitano vilivyopo katika mitaa ya Mji mpya, Chamwino, Kichangani na Misongeni.
 
Aliwataka wakazi wa Morogoro kuhakikisha wanawazuia watoto wao kuangalia picha hizo kwa kuwa zinawafundisha maadili yasiyofaa.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.