Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Fuvu la mtu aliyeuawa ’Februari’ lagunduliwa
Fuvu la mtu aliyeuawa ’Februari’ lagunduliwa
By Habari Tanzania | Published  07/17/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Mabaki ya mtu anayedaiwa kuuawa takriban miezi mitano iliyopita, yamekutwa katika kijiji cha Mbangamawe mkoani Ruvuma, kando kando ya barabara iendayo Njombe.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Ruvuma, Bw. Falhum Mshana, alisema mabaki hayo yaligunduliwa baada ya raia wema kutoa taarifa polisi.

Kamanda Mshana alisema masalia yaliyokutwa eneo hilo ni fuvu la kichwa, mifupa na nguo za kike, jambo linaloashiria kuwa, marehemu huyo alikuwa ni mwanamke anayekadiriwa kuwa na umri wa miaka kati ya 20 na 26.

Kadhalika, alisema katika eneo la tukio, ilikutwa damu iliyoganda ikiwa imetapakaa.
Kamanda Mshana aliongeza kuwa, uchunguzi wa awali uliofanywa na daktari umebaini kuwa, marehemu alifariki dunia takriban miezi mitano iliyopita.

Alisema polisi wanaendelea kufanya uchunguzi wa tukio hilo na kwamba mpaka sasa, hakuna mtu aliyekamatwa kuhusiana na tukio hilo.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.