Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Daktari Muhimbili matatani
Daktari Muhimbili matatani
By Habari Tanzania | Published  07/14/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Mwandishi Wetu

POLISI mkoani Dar es Salaam, inamsaka daktari wa kike wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa tuhuma za kuandika ujumbe (SMS) wa matusi kwa mke wa wakili wa kujitegemea (jina limehifidhiwa).

Polisi imefikia hatua ya kumsaka daktari hiyo baada ya  mke wa wakili huyo kutoa malalamiko hayo katika Kituo cha Polisi cha Oysterbay, Dar es Salaam.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Kamishna Afred Tibaigana, alisema jana kuwa mke wa wakili huyo amefungua kesi yenye namba OB/RB/11740/06 katika kituo cha polisi cha Oysterbay na taarifa hizo kufikishwa Kituo Kikuu cha Polisi.

“Ni kweli tumepata malalamiko, na meseji hizo za matusi na kashfa tumezisoma, kwa bahati nzuri daktari huyo anatumia mtandao wa Tigo, kwa hiyo tunafuatilia kuweza kujua ni nani na anapatikana wapi,” alisema Tibaigana.

Hata hivyo, habari ambazo Tanzania Daima imezipata, zinasema kuwa daktari huyo anadaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wakili huyo.

“Tunamwita wakili huyo tuzungumze naye, tujue kama kweli wana uhusiano na daktari huyo, na yeye atatusaidia kumpata kwani hatutarajii kwa mwanamke huyo msomi awe na tabia hiyo,” alisema Tibaigana.

Alipohojiwa na Tanzania Daima, mke wa wakili huyo alisema anahisi daktari huyo ana uhusiano wa kimapenzi na mumewe.

Alisema ni kawaida kwa daktari huyo kumtukana na kumtishia kwamba ataachika na yeye atachukua nafasi yake.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.