Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  TPSF yamwomba Kikwete airudishe nchi COMESA
TPSF yamwomba Kikwete airudishe nchi COMESA
By Habari Tanzania | Published  07/14/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Kulwa Karedia

TAASISI ya Sekta Binafsi Tanzania (TPSF), imemuomba Rais Jakaya Kikwete, kuirudisha Tanzania kwenye uanachama wa Jumuia ya Uchumi ya nchi za Mashariki na Kusini mwa Afrika (COMESA) ili kujenga uchumi bora wa nchi.

Kauli hiyo ilitolewa juzi na Mwenyekiti wa taasisi hiyo Elvis Musiba, wakati alipokuwa akifunga warsha ya siku moja ya wadau mbalimbali wa mambo ya uchumi, katika Hoteli ya Movenpick iliyokuwa inajadili athari za Tanzania kujitoa uanachama kwenye jumuiya hiyo.

 “Tunamuomba Rais Jakaya Kikwete atumie busara zake zote kuhakikisha Tanzania inarudi tena kuwa mwanachama wa COMESA ili tuweze kujenga uchumi wa nchi, hasa kwa wenye viwanda,” alisema Musiba.

Alisema si kweli kwamba viwanda vingi nchini vimeshindwa kuuza bidhaa katika soko la COMESA kwa madai kuwa viko chini ya viwango vinavyohitajika kimataifa.

Musiba alisema nchi zote zilizoko kwenye Jumuiya ya Uchumi ya Kusini mwa Afrika (SADC) ni wanachama wa COMESA, hivyo itakuwa jambo la aibu kwa Tanzania kujitoa, kwani kufanya hivyo ni sawa na kuwafungia wafanyabishara soko lao.

Alisema siku zote Rais Kikwete amekuwa mstari wa mbele kuzitaka taasisi zisizokuwa za kiserikali na wamiliki wakubwa wa viwanda kuhakikisha wanakuwa mbele katika kupandisha uchumi wa Tanzania.

Naye Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyabiashara Afrika Mashariki  (EABC), Arnold  Kilewo alisema umefika wakati sasa wa Tanzania kuamua mambo yake kwa ajili ya manufaa ya watu wake.

Alisema kutegemea soko la Jumuiya ya Afrika Mashariki peke yake halitaisaidia zaidi kama bidhaa nyingi zinazozalishwa hapa nchini hazitasafirishwa nje ya nchi


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.