Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Ushauri wa Lowassa kwa KKKT
Ushauri wa Lowassa kwa KKKT
By Habari Tanzania | Published  07/12/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
Na Omari Shaaban, Arumeru
 
WAZIRI Mkuu Edward Lowassa amewataka wajumbe wa mkutano mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), kuhakikisha wanamchagua askofu atakayedumisha amani, mshikamano na upendo ndani ya kanisa hilo na siyo atakayekuwa kama ugonjwa wa polio katika utendaji wake wa kazi.
 
Lowassa aliwataka wajumbe ambao wapo kwenye mkutano wao mkuu wa 17, kujiepusha na migawanyiko yoyote itakayoweza kuukumba uchaguzi huo.
 
Mkutano utamchagua askofu mpya wa kuliongoza kanisa hilo baada ya wa sasa, Askofu Samson Mushemba, kumaliza muda wake keshokutwa.
 
Akizungumza jana kwenye ufunguzi wa mkutano huo, unaofanyika katika Chuo Kikuu Kishiriki cha Tumaini, kilichopo Makumira wilayani Arumeru, Waziri Mkuu alisema kuwa katika uchaguzi mbalimbali wa kisiasa kunakuwepo na migawanyiko ya makundi, lakini hiyo haipaswi kujitokeza katika uchaguzi wa kidini, kutokana na kugusa imani zaidi badala ya siasa.
 
Waziri Mkuu alisema kuwa madhehebu ya dini na asasi zake yanafanya jitihada kubwa katika kuwaletea wananchi maendeleo, ikiwemo kujenga shule, huduma za matibabu, shughuli za maendeleo ya kawaida kama upatikanaji wa barabara, maji na utunzaji wa mazingira.
 
Lowassa, ambaye pamoja na kufungua mkutano pia alizindua chuo hicho kikuu kishiriki, alisema kuwa uzinduzi huo ni kielelezo tosha cha mchango wa makanisa, katika maendeleo ya taifa, hususan katika sekta ya elimu.
 
Alisema vyuo vikuu vinapaswa kujiimarisha katika mafunzo na kufanya utafiti mbalimbali na kusambaza matokeo yake kwa jamii, kwa lengo la kuwaondolea wananchi umaskini.
 
Serikali, alisema, inatambua umuhimu wa mchango wa sekta binafsi katika kukuza elimu nchini, na kwamba mpaka sasa Tanzania ina vyuo vikuu vya umma na binafsi vinavyofikia 30, vyenye wanafunzi 36,870, na asilimia 14 ya wanafunzi hao wapo kwenye vyuo vikuu binafsi.
 
Waziri Mkuu alisema kuwa KKKT hapa nchini imekuwa mstari wa mbele katika kuchangia sekta ya elimu, na mpaka sasa ina shule za sekondari zaidi ya 50, za ufundi zaidi ya 20, vyuo vya ualimu viwili na chuo kikuu kimoja chenye vyuo vishiriki vitatu.
 
Leo Rais mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, anatazamiwa kutoa mada kwenye mkutano huo kuhusu utandawazi na uwekezaji.

How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.