Kitaifa
   Siasa
   Jamii
   Uchumi
   Makala

 

Search


Advanced Search

 »  Home  »  Habari za Kitaifa  »  Lundenga amfagilia Manji
Lundenga amfagilia Manji
By Habari Tanzania | Published  07/4/2006 | Habari za Kitaifa | Unrated
na Khadija Kalili

MMOJA wa viongozi wa kundi la wanachama wa Yanga, maarufu kama ‘Yanga Family’, Hashim Lundenga amempongeza Mkurugenzi wa Quality Group, Yussuf Manji, kwa mikakati yake ya kuiboresha timu ya Yanga akiwa na mipango ya kutaka kuleta kocha mpya.

Akizungumza jana Dar es Salaam, Lundenga alisema kwamba wanachama na viongozi wa Yanga hawana budi kumpa ushirikiano Manji ili kuiweka timu hiyo katika mikakati ya kusaka ubingwa katika ngazi ya kimataifa.

“Nimefurahishwa  sana kusikia  Manji analeta Kocha,  ni jambo zuri sana, Yanga imecchukua ubingwa  mara nyingi hapa nchini kuizidi timu ya Simba na timu nyingine, hivyo tuitumie nafasi hii katika kujiimarisha kisoka,” alisema Lundenga.

Alisema kwamba kwa hilo la kumleta kocha, mdhamini huyo ameona mbali na kwamba kundi la wanachama wa Yanga Family litaendelea na harakati zake za kuleta maendeleo, na kamwe halitabweteka na udhamini wa Manji.


How would you rate the quality of this article?
1 2 3 4 5
Poor Excellent
Add comment
Comments


Article Options
This article has been added to your 'Articles to Read' list.
Your Favorite Articles
View All Favorites
Articles to Read
You Recently Viewed...
Popular Articles
  1. Unaifahamu Jambo Forums?
  2. Barua ya Wazi kwa Rais Jakaya Kikwete
  3. Ghorofa Jijini lanusurika kuungua moto
  4. Is Tanzania a safe place to invest?
  5. Britsh M.P. calls for the suspension of aid to Tanzania.
No popular articles found.
Popular Authors
  1. Habari Tanzania
  2. Mzee Mwanakijiji
  3. Marshy Abdu
  4. Linda Garner
  5. Nthelezi Nesaa
  6. Prosper Kwigize
  7. Ramadhan Semtawa
  8. Salehe Mmoro
  9. Manyerere Jackton
  10. Ndesanjo Macha
No popular authors found.